Jarida la Kilimo, Julai - Septemba, 2011
Jarida la Kilimo, Julai - Septemba, 2011
Jarida la Kilimo, Julai - Septemba, 2011
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Toleo <strong>la</strong> Saba<br />
ISSN: 1821-8113 Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza <strong>la</strong> Mapinduzi Mhe: Dkt. Ali Mohamed Shein wa pili<br />
kutoka kushoto pomoja na viongozi wengine akiwa katika harakati za uvunaji wa mpunga wa<br />
mbegu aina ya NERICA kituo cha uzalishaji wa mbegu Bambi, Wi<strong>la</strong>ya ya Kati Unguja.<br />
Yaliyomo<br />
Maoni ya Mhariri/Picha ya Ja<strong>la</strong>da...........................................................................Uk.2<br />
Uvunaji na Uanikaji wa Karafuu............................................................................Uk.3 - 4<br />
Upotevu wa Rutuba na Urutubishaji wa Ardhi.......................................................Uk.4 - 5<br />
Uvunaji na Uanikaji wa Karafuu..............................................................................Uk.6 - 7<br />
Matukio katika Picha.............................................................................................Uk.8 - 9<br />
Mabaraza ya Wakulima..........................................................................................Uk.10<br />
Athari za Joto kwa Mifugo...............................................................................Uk.11 - 12<br />
Mbinu Bora za Ujasiriamali..............................................................................Uk.13 - 14<br />
Umuhimu wa Rasilimali za Msituni......................................................................Uk. 15 - 16
Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong> WAHARIRI/MAONI/PICHA YA JARIDA<br />
Bodi ya Wahariri MAONI YA MHARIRI<br />
Washauri<br />
Affan O. Maalim<br />
Juma Ali Juma<br />
Dk. Bakar S. Asseid<br />
Mhariri Mkuu<br />
Dk. Juma M. Akil<br />
Msanifu na Mhariri<br />
Mtendaji<br />
Hashim H. Chande<br />
Wahariri Wasaidizi<br />
Makame M. Abdulrahman<br />
Nassor S. Mkarafuu<br />
Nassor S. Mohammed<br />
Mpiga chapa<br />
Fatma A. Juma<br />
Mpiga picha<br />
Khamis A. Bakari<br />
ANUWANI<br />
Wizara ya <strong>Kilimo</strong>,<br />
Maliasili - Zanzibar<br />
S.L.P. 159<br />
Simu: +255 24 2230986<br />
Fax: +255 24 2234650<br />
E-mail: kilimo@zanlink.com<br />
Tovuti: kilimoznz.or.tz<br />
Ndugu wakulima, kupata chaku<strong>la</strong> cha kutosha na kilicho<br />
bora kwa ki<strong>la</strong> mwananchi ni sua<strong>la</strong> gumu ambalo linahitaji<br />
mipango na mikakati mizuri ya serikali kupitia Wizara<br />
husika. Moja ya tatizo kubwa linalowakabili wananchi ni<br />
kuchelewa kukamilisha hatua za mwanzo za matayarisho ya<br />
mashamba, kulima eneo kubwa ambalo hawana uwezo nalo<br />
na kutokutumia zana na pembejeo bora za kilimo.<br />
Ndugu wakulima, moja ya kikwazo kikubwa ni uwezo mdogo<br />
wa kutumia zana bora za kilimo, mbegu bora, mbolea na<br />
kutozingatia kanuni na taaluma bora za uzalishaji ambazo<br />
zinatolewa na Wizara ya <strong>Kilimo</strong> na Maliasili. Vikwazo hivi<br />
humsababishia mkulima kutumia nguvu nyingi, muda<br />
mrefu na kupata mavuno hafi fu na tija ndogo.<br />
Ndugu wakulima, kwa miaka mingi neno “Ukulima wa<br />
Kisasa” limekuwa ni wimbo <strong>la</strong>kini bado mkulima wa visiwani<br />
anategemea zana na pembejeo duni kama vile mbegu na<br />
jembe <strong>la</strong> mkono (kijembe kongoroka). Serikali ya Mapinduzi<br />
ya Zanzibar kupitia Wizara ya <strong>Kilimo</strong> na Maliasili inafanya<br />
mabadiliko makubwa katika kilimo ili kukifanya kilimo hicho<br />
kiwe katika mfumo wa kisasa “Mapinduzi ya <strong>Kilimo</strong>”.<br />
Ndugu wakulima, katika kufanikisha sua<strong>la</strong> hili Serikali<br />
imeongeza upatikanaji wa pembejeo na zana za kilimo<br />
yakiwemo matrekta makubwa na madogo, mbegu bora na<br />
mbolea, kuongeza usamabazaji wa taaluma kwa wakulima<br />
kwa kuongeza idadi ya mabwana/mabibishamba katika<br />
shehia pamoja na kutoa ruzuku ya aslimia 75% kwa kazi za<br />
utayarishaji wa mashamba na ununuzi wa mbegu bora na<br />
mbolea.<br />
Ndugu wakulima, hatunabudi kuunga mkono juhudi hizi<br />
za Serikali ili kufanikisha azma ya “Mapinduzi ya <strong>Kilimo</strong>”<br />
hivyo tunaipongeza na tunaiomba iendelee na juhudi zake<br />
za kuwashajiisha na kuwashirikisha wakulima kikamilifu<br />
katika kupanga malengo yao juu ya mpango wa utumiaji wa<br />
zana na pembejeo bora za kilimo.<br />
Ndugu wakulima, kwa kuunga mkono juhudi hizi za Serikali,<br />
Wizara ya <strong>Kilimo</strong> na Maliasili itaendelea kutoa mafunzo ya<br />
utumiaji bora wa zana na pembejeo za kilimo na kuweka<br />
mpango maalumu ya mafunzo kwa ki<strong>la</strong> shehia juu ya<br />
umuhimu wa zana hizo pamoja na matumizi yake ili kufi kia<br />
lengo <strong>la</strong> wakulima katika kujitosheleza kwa chaku<strong>la</strong>, kuinua<br />
hali zao za maisha na kuipunguzia mzigo Serikali wa kuagiza<br />
chaku<strong>la</strong> kutoka nje ya nchi.<br />
PICHA YA JALADA<br />
Katika picha anaonekana Rais wa Zanzibar Mhe. Ali Mohamed Shein<br />
akivuna mpunga wa mbegu aina ya NERICA katika shamba <strong>la</strong> kuzalisha<br />
mbegu liliopo Bambi pamoja nae kutoka kulia kwake ni Waziri wa<br />
<strong>Kilimo</strong> na Maliasili Mhe, Mansoor Y. Himid, Mkuu wa Mkoa wa Kusini<br />
(U) Mhe, Mustafa Ibrahim na Naibu Katibu Mkuu (kilimo) ndugu Juma<br />
A. Juma, tarehe 7 Ju<strong>la</strong>i <strong>2011</strong>.<br />
2
MAZAO BORA Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />
ILI TUVUNE MAZAO BORA NI LAZIMA TUPANDE<br />
MBEGU BORA ZINAZOWEZA KUTUPATIA TIJA<br />
Na Sabiha H. Saleh<br />
Mnamo tarehe 2/7/<strong>2011</strong> Rais<br />
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa<br />
Baraza <strong>la</strong> mapinduzi Mhe. Dkt. Ali<br />
Mohammed Shein aliyasema hayo<br />
kwa nyakati tofauti aliposhiriki<br />
kikamilifu katika uzinduzi wa Kitaifa<br />
wa uvunaji wa mbegu ya mpunga aina<br />
ya “NERICA”, huko Bambi na bonde<br />
<strong>la</strong> Kisima Mchanga liliopo Kiboje<br />
Mkwajuni Wi<strong>la</strong>ya ya Kati Unguja.<br />
Hii ni hatua mojawapo ya Serikali ya<br />
mapinduzi ya Zanzibar katika jitihada<br />
zake za kukuza na kuendeleza kilimo<br />
kwa ujum<strong>la</strong>.<br />
Dkt. Shein amesema kuwa lengo kuu<br />
<strong>la</strong> Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar<br />
kufanya mapinduzi ya kilimo tayari<br />
limeanza kutekelezwa na mbegu<br />
aina ya NERICA ndio mkombozi wetu<br />
kwani Serikali itaendelea kuchukua<br />
ki<strong>la</strong> jitihada kuona kuwa wakulima wa<br />
Zanzibar wananufaika na kilimo chao<br />
pamoja na taifa kwa ujum<strong>la</strong>.<br />
Alisema kuwa azma ya Serikali kwa<br />
upande wake ni kuona kuwa Mapinduzi<br />
ya kilimo yanaleta tija kwa wakulima<br />
pamoja na wananchi kwa ujum<strong>la</strong> kwa<br />
kuweza kupata kile kilichokusudiwa.<br />
Aidha, amefahamisha kuwa nia na<br />
dhamira ni kuwainua wakulima na<br />
Serikali inaendelea na taratibu za<br />
kuwaletea wakulima wake mashine<br />
za kuvunia mpunga, kuwapunguzia<br />
bei za pembejeo pamoja na kuwapatia<br />
matrekta kwa ajili ya kuvurugia na<br />
dawa za kuulia wadudu ili mkulima<br />
aweze kumudu gharama za uendeshaji<br />
na tuweze kulima kwa tija zaidi.<br />
Akizungumzia kuhusiana na mfumko<br />
wa bei za vyaku<strong>la</strong> hasa mchele ambao<br />
ndio chaku<strong>la</strong> kikubwa kwa watu wa<br />
Zanzibar amesema kuwa Serikali tayari<br />
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza <strong>la</strong> Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed<br />
Shein aliyesimama na shuke <strong>la</strong> mpunga akiwa katika uzinduzi wa uvunaji wa mbegu<br />
ya mpunga aina ya NERICA katika Shamba <strong>la</strong> Uzalishaji wa mbegu Bambi<br />
imeshaanza kutekeleza mapinduzi ya<br />
kilimo kwa kupambana na hali hiyo.<br />
Akifafanua zaidi kuhusu ongezeko <strong>la</strong><br />
Idadi ya Watu duniani, kwa upande wa<br />
Zanzibar amesema tokea Mapinduzi<br />
Matukufu ya Januari mwaka 1964<br />
ambapo idadi ya watu ilikuwa 320,000<br />
hadi mwaka 1974 ilikuwa ni 640,000<br />
na kwa mujibu wa takwimu ya sensa<br />
ya mwaka 2002 ambapo ilifi kia watu<br />
milioni 1.2 idadi ambayo inapelekea<br />
ongezeko <strong>la</strong> mahitaji ya chaku<strong>la</strong>.<br />
Kutokana na ongezeko <strong>la</strong> watu ,<br />
takwimu zinaonyesha kwamba mchele<br />
unaotumiwa kwa chaku<strong>la</strong> hapa<br />
Zanzibar ni tani 80,000 kwa mwaka,<br />
unaozalishwa na wakulima ni chini ya<br />
tani 16,000 na kiasi chote kilichobaki<br />
hununuliwa kutoka nje ya nchi. Aidha,<br />
Dkt. Shein alisisitiza haja ya kuongeza<br />
uzalishaji wa chaku<strong>la</strong>.<br />
Pia aliwataka wakulima kufuata<br />
ushauri wa wata<strong>la</strong>mu na kubadilika ili<br />
kilimo chetu kiwe cha kisasa. Hivyo,<br />
hatuna budi kutumia teknolojia ya<br />
3<br />
kisasa na kuweza kujitegemea katika<br />
kilimo cha mpunga kwa anga<strong>la</strong>u<br />
asilimia 60, “Ukitumia mbegu bora<br />
unaweza kuvuna mavuno bora”.<br />
Amefahamisha kuwa kulima kwa<br />
kutumia mbegu bora kunapelekea<br />
kuvuna mazao mengi na bora, hivyo<br />
tuongeze jitihada na kukifanya chaku<strong>la</strong><br />
kuongezeka.<br />
Aidha Dkt. Shein amesema kuwa<br />
Washirika wa Maendeleo wako tayari<br />
na wanaendelea na jitihada za kuiunga<br />
mkono Zanzibar katika Sekta ya <strong>Kilimo</strong><br />
wakiwemo, Korea ya Kusini, Marekani,<br />
Japan hasa katika mradi wao wa ‘Feed<br />
the Future’.<br />
Akiwa katika bonde <strong>la</strong> Kisima<br />
Mchanga, Dkt. Shein aliwaahidi<br />
wakulima kuwajengea njia yao kwa<br />
kiwango cha kifusi kutoka barabara<br />
kuu hadi bondeni, kuwawekea umeme,<br />
kuwachimbia kisima na kuwapatia<br />
tre<strong>la</strong> <strong>la</strong> kubebea mizigo.<br />
Akimkaribisha Rais wa Zanzibar
Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong> UPOTEVU WA RUTUBA NA URUTUBISHAJI ARDHI<br />
Waziri wa <strong>Kilimo</strong> na Maliasili Mhe.<br />
Mansoor Yussuf Himid amesema kuwa<br />
Mapinduzi ya <strong>Kilimo</strong> ni mageuzi ya<br />
haraka yalioendelevu katika kukipa<br />
nguvu zaidi kilimo pamoja na wakulima<br />
kwani faida inayopatikana huwa ni kwa<br />
taifa zima.<br />
Amefahamisha kuwa hali ya Ulimwengu<br />
imebadilika na sisi <strong>la</strong>zi tubadilike tuwe<br />
na mikakati imara katika kukibadilisha<br />
kilimo chetu kwa faida ya nchi yetu.<br />
Alisema kuwa dhamira ya Wizara ya<br />
<strong>Kilimo</strong> na Maliasili ndani ya miaka<br />
mitano ni kulima hekta 6,000 za<br />
umwagijiliaji maji, kati ya hekta<br />
8,521 ambapo kwa sasa ni hekta<br />
700 tu ndizo zinazolimwa. Aidha,<br />
alifahamisha kuwa Jamhuri ya Korea<br />
ya Kusini imeahidi kusaidia kulima<br />
hekta 2,000 na Serikali ya Marekani<br />
hekta 2,000.<br />
Aliongeza kusema kuwa mashamba<br />
UPOTEVU WA RUTUBA NA NJIA<br />
ZA KURUTUBISHA ARDHI<br />
Na Hashim H. Chande<br />
Ardhi yenye rutuba ni muhimu<br />
katika ukuwaji wa mimea na<br />
upatikanaji wa mavuno yaliyo bora.<br />
Kama tunavyoelewa kuwa rutuba<br />
ni chaku<strong>la</strong> cha mimea ambacho<br />
kinapatikana kwenye udongo. Ili<br />
kuuweka udongo katika hali ya<br />
rutuba na kuiwezesha mimea<br />
iendelee kukua vizuri ardhini hatuna<br />
budi kutumia mbolea ili kurudisha<br />
chaku<strong>la</strong> kilichochukuliwa na mimea.<br />
Mbolea zinatumika kuongeza<br />
rutuba na kuiwezesha ardhi kutoa<br />
mazao mengi, kinachohitajika ni<br />
jinsi ya kujua aina gani ya mbolea,<br />
kiwango, na wakati zinapohitajika.<br />
Hivyo Mabwana/mabibi shamba<br />
waliomo katika maeneo ya kilimo<br />
wanajukumu <strong>la</strong> kuwaelimisha<br />
wakulima wa sehemu hizo.<br />
Tishio <strong>la</strong> upoteaji wa rutuba<br />
darasa yataongezwa hadi kufi kia<br />
1,200, pia mashamba darasa manne<br />
ya mikarafuu yataanzishwa, mawili<br />
Unguja na mawili Pemba.<br />
Mhe. Waziri wa <strong>Kilimo</strong> aliwaeleza<br />
wakulima kuwa katika bajeti ya Wizara<br />
ya mwaka <strong>2011</strong>/2012 itakuwa na<br />
matumaini kwa wakulima wa visiwa<br />
hivi.<br />
Nae Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja<br />
Mhe. Mustafa Muhammed Ibrahim<br />
aliwatoa hofu wakulima wa bonde<br />
<strong>la</strong> Kisimamchanga na kuwataka<br />
kuendelea kulitumia bonde hilo kwani<br />
tayari limeshapimwa na Wizara ya<br />
<strong>Kilimo</strong> kwa lengo <strong>la</strong> kuanza kilimo cha<br />
umwagiliaji maji.<br />
Nao wakulima wa bonde <strong>la</strong><br />
Kisimamchanga wameushukuru mradi<br />
wa PADEP uliotumia zaidi ya shilingi<br />
milioni 32 ambao umeleta mafanikio<br />
makubwa kwa kuongeza uzalishaji<br />
Ardhi iliyopoteza rutuba imeshambuliwa na ukame na hutoa mazao hafi fu au kutoweza<br />
kutoa mazao ya aina yoyote.<br />
4<br />
kutoka polo 4 kwa robo hekta kwa<br />
sasa, wakati hapo zamani walikuwa<br />
wakizalisha polo 4 kwa hekta nzima.<br />
Jum<strong>la</strong> ya hekta 5 za mbegu ya mpunga<br />
wa aina ya ‘NERICA’ zimevunwa na<br />
zinatarajiwa kupandwa kwa wingi<br />
katika msimu wa mvua za vuli zijazo<br />
kwa lengo <strong>la</strong> kupandwa wakati wa<br />
masika ambapo zinatarajiwa zaidi ya<br />
tani 3,700 kupatikana katika msimu<br />
ujao wa masika ili kufi kia asilimia 50%<br />
ya uzalishaji ndani ya miaka mitano.<br />
Uzinduzi huo wa kitaifa uliwashirikisha<br />
viongozi kutoka Mikoa 5 ya Unguja<br />
na Pemba, wakiwemo Mawaziri,<br />
Wawakilishi, Mkuu wa Mkoa wa Kusini<br />
ambaye ndiye mwenyeji wa shughuli<br />
hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mjini/<br />
Magharibi, Mkuu wa Mkoa wa Kusini<br />
Pemba, Viongozi wa Serikali pamoja<br />
na Wakisiasa na wananchi kutoka<br />
maeneo mbalimbali.
UPOTEVU WA RUTUBA NA URUTUBISHAJI ARDHI Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />
Mchanganyiko wa vitu tofauti vilivyotumika katika kutengenezea mboji ikiwemo<br />
majani, udongo, takataka, mabaki ya mimea na maji.<br />
katika udongo<br />
Katika nchi yetu tumekabiliwa na<br />
tishio kubwa <strong>la</strong> kupoteza rutuba<br />
ya udongo kutokana uharibifu wa<br />
mazingira unaosababishwa na<br />
ukataji wa miti ovyo, kuchimba<br />
mchanga, kuchimba na kukata<br />
matofali ya mawe na kilimo<br />
kisichozingatia kanuni bora.<br />
Ardhi inayotumiwa vibaya kwa kilimo<br />
pasi na kurudishia rutuba yake<br />
ni chanzo kikubwa cha upotevu<br />
wa rutuba hiyo ya asili ambayo ni<br />
chaku<strong>la</strong> muhimu cha mimea na<br />
viumbe vyengine vinavyoishi katika<br />
udongo. Upungufu huo husababisha<br />
udongo kupunguza uwezo wake wa<br />
kuhifadhi maji kwa muda mrefu<br />
ambapo ukame hutokea na mazao<br />
yanayopandwa kutoa mavuno<br />
hafi fu.<br />
Rutuba hiyo ni <strong>la</strong>zima irudishwe<br />
ili tuweze kupata tena mavuno<br />
bora. Hivyo, tunapaswa kuzingatia<br />
urutubishaji wa ardhi kwa kuweka<br />
viwango sahihi vya mbolea<br />
kulingana na mahitaji halisi ya<br />
mimea iliyopandwa, kwa mfano<br />
mpunga unahitaji kiasi cha kilo 100 -<br />
150 cha mbolea kwa ki<strong>la</strong> ekari mbili<br />
na nusu (2.5). Kwa wale wakulima<br />
wenye tabia ya kupumzisha ardhi<br />
kwa kipindi cha mwaka mmoja au<br />
miwili kwa kuchunga wanyama au<br />
kuweka mazizi katika maeneo hayo<br />
wakati wa kupumzisha ardhi, njia hii<br />
husaidia kurudisha rutuba ardhini<br />
ijapokuwa hivi sasa haitumiki sana<br />
katika maeneo mengi kutokana<br />
na ongezeko kubwa <strong>la</strong> mahitaji ya<br />
ardhi.<br />
Kutokana na ongezeko <strong>la</strong> mahitaji ya<br />
matumizi ya mbolea za viwandani na<br />
gharama kubwa za upatikanaji wake,<br />
wakulima hatuna budi kujitengezea<br />
mbolea sisi wenyewe kwa kutumia<br />
malighafi tulizonazo kama vile<br />
kupanda mazao ya jamii ya kunde,<br />
matumizi mboji na samadi.<br />
UTENGENEZAJI WA MBOLEA YA<br />
MBOJI<br />
Ili kudumisha uzalishaji wa chaku<strong>la</strong>,<br />
wakulima wa Zanzibar wanasisitizwa<br />
kutengeneza na kutumia mbolea<br />
ya samadi, mboji na takataka pale<br />
ambapo zinapopatikana kwa urahisi.<br />
Mbolea hizi mbali ya kurutubisha<br />
ardhi, pia husaidia kuifanya ardhi<br />
iwe katika hali nzuri iliyoshikamana.<br />
Ingawa wakulima wanahimizwa<br />
kutumia mbolea za viwandani kwa<br />
baadhi ya mazao, <strong>la</strong>kini sirahisi<br />
kufi dia pengo <strong>la</strong> mbolea yote<br />
inayohitajika kwa wakati huu ambao<br />
ardhi inaonyesha kuchoka, kutokana<br />
na matumizi mabaya ya mfululizo.<br />
Kupuuza mbolea hizi kunaweza<br />
kuleta madhara makubwa katika<br />
kilimo.<br />
5<br />
Mbolea ya mboji ni mchanganyiko<br />
wa mabaki ya vitu vyenye asili ya<br />
uhai ambavyo hukusanywa kutoka<br />
mashambani na majumbani kama<br />
vile takataka, mabua ya mimea,<br />
magugu, vinyesi vya wanyama au<br />
hata mbolea ya chumvi chumvi.<br />
FAIDA YA MBOLEA YA MBOJI<br />
• Hukaa ardhini na hutumiwa na<br />
mimea kwa muda mrefu, kuliko<br />
mbolea ya chumvi.<br />
• Mboji ina uwezo wa kubadili hali<br />
ya udongo na kuufanya utumike<br />
kwa kilimo.<br />
• Mboji inawezesha udongo<br />
kuhifadhi unyevu kwa muda<br />
mrefu.<br />
• Mboji ni rahisi kutengeneza,<br />
kutumiwa na haina gharama<br />
kubwa ukilinganisha na mbolea<br />
za viwandani.<br />
JINSI YA KUTENGENEZA<br />
i Safi sha eneo unalotaka<br />
kutengeneza mbolea.<br />
ii Pima mita 1.5 urefu na mita 1.5<br />
upana na weka fi to baada ya<br />
kupima urefu na upana, urefu<br />
wa fi to unategemea mahitaji ya<br />
mkulima.<br />
iii Chimbua chimbua na weka vizuri<br />
udongo.<br />
iv Panga tabaka <strong>la</strong> udongo, majani,<br />
mabua na kuyatandaza pamoja<br />
na takataka zinazoweza kuoza.<br />
iii Weka tabaka <strong>la</strong> udongo wa<br />
kutosha juu mabua na majani<br />
kwa mpangilio.<br />
iv Tumia mbolea ya chumvi chumvi<br />
au vinyesi vya wanyama kwa<br />
kunyunyizia juu ya udongo.<br />
v Nyunyizia maji baada ya kuweka<br />
mbolea, kwa kumalizia tabaka <strong>la</strong><br />
kwanza. Rudia kuweka tabaka <strong>la</strong><br />
pili mpaka <strong>la</strong> tatu juu yake kwa<br />
kufata mpangilio ule ule wa<br />
tabaka <strong>la</strong> mwanzo hadi kufi kia<br />
urefu wa mita 1-2.<br />
vi Hakikisha tabaka lina unyevu na<br />
joto <strong>la</strong> kutosha. Geuza tabaka<br />
hizo ki<strong>la</strong> baada ya wiki mbili<br />
kwa kupunguza hewa na unyevu<br />
uliozidi ili kuozesha takataka<br />
kikalifu.<br />
vii Mbolea hiyo inatakiwa itumike<br />
baada ya kuoza na kupoa.
Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong> KARAFUU<br />
UVUNAJI NA UANIKAJI KARAFUU<br />
Na Rashid Khamis<br />
Zanzibar imekuwa ikijulikana<br />
sana katika uuzaji wa karafuu<br />
bora kuanzia karne ya 18, karafuu<br />
bora zinapatikana kutoana na<br />
uchumaji, uchambuaji, uanikaji<br />
bora pamoja na usafi shaji wa<br />
karafuu kab<strong>la</strong> ya kuuza. Katika<br />
miaka ya 2000 tumeshuhudia<br />
kurejeshwa kwa uchafu wa<br />
karafuu zilizouzwa nje katika<br />
Shirika <strong>la</strong> Biashara <strong>la</strong> Taifa<br />
<strong>la</strong> Zanzibar (ZSTC) Hali hii<br />
inasababisha Zanzibar kupoteza<br />
sifa yake ya kuuza karafuu bora.<br />
UVUNAJI<br />
Karafuu nzuri kwa biashara<br />
ni yenye rangi kutoka kijani<br />
na kuingia rangi ya manjano<br />
kab<strong>la</strong> ya kuchanua. Karafuu<br />
ikachanua inabadilika na kuwa<br />
mbegu na hupoteza matumizi<br />
yaliyokusudiwa.<br />
Wakati wa uchumaji wa karafuu ni<br />
vizuri kuepuka ukataji wa matawi<br />
kwani tabia hii hudhoofi sha<br />
mikarafuu na husababisha<br />
kushambuliwa na maradhi na<br />
hatimae kufa.<br />
Mwananchi akiwa katika harakati za kuvuna karafuu ili kuliokoa zao hili<br />
<strong>la</strong> kitaifa lisipotee<br />
Wakati wa kuchuma, matawi<br />
dhaifu ya mikarafuu mikubwa<br />
yafungwe pamoja kwa kutumia<br />
kamba. Aidha Hii itasaidia<br />
kufanya yawe madhubuti zaidi,<br />
hivyo kupunguza uwezekano wa<br />
kukwanyuka kutokana na uzito<br />
wa mchumaji. Kamba au vingoe<br />
Mwanamama akiwa mstari wa mbele katika kushiriki kuchambua<br />
karafuu kwa lengo <strong>la</strong> kuliokoa zao hili <strong>la</strong> Taifa<br />
6<br />
vitumike kwa kuvuta matawi<br />
yaliyombali ili yaweze kuchumwa<br />
kirahisi bada<strong>la</strong> ya kuyavunja.<br />
Mikarafuu midogo inaweza<br />
kuchumwa kwa kutumia ngazi na<br />
hii inasaidia kupunguza kwa kiasi<br />
kikubwa uharibifu huo.<br />
UANIKAJI<br />
Karafuu zianikwe haraka baada<br />
ya kuchambuliwa na kusafi shwa<br />
na hakikisha sehemu za kuanikia<br />
zinapata jua wakati wote (kutwa<br />
nzima). Usianike karafuu karibu<br />
na jengo lolote au miti mirefu<br />
inayoweza kutoa kivuli.<br />
Miongoni mwa vifaa vilivyo bora<br />
kwa kuanikia karafuu ni majamvi<br />
kwa sababu huhifadhi karafuu<br />
vizuri zaidi wakati wa mvua<br />
kuliko aina nyengine za vifaa<br />
kama magunia. Magunia yakiroa<br />
hufyonza maji na kurowesha<br />
karafuu, pia hupunguza gredi<br />
kwa kutoa nyuzi ambazo<br />
huchanganyika na karafuu.<br />
Karafuu zinazoanikwa juu ya<br />
sakafu ziendelee kuwekwa kwenye<br />
majamvi kwa vile sakafu huchuna
KARAFUU Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />
karafuu wakati wa kugeuza na<br />
kuanua. Inashauria majamvi<br />
yawekwe juu ya majani mafupi<br />
kuepuka kuingia vumbi. Haitakiwi<br />
kuanika karafuu pembezoni mwa<br />
barabara ili kuepusha kupoteza<br />
ubora wake kwa kuchanganyika<br />
na vitu vengine, kupondwa na gari<br />
au kukanyagwa na wapita njia.<br />
Karafuu bora zinatakiwa ziwe na<br />
sifa zifuatazo:<br />
• Ziwe hazina vitawi, vijiti na<br />
matende nzima na zenye<br />
umbo <strong>la</strong> namna moja<br />
zisizoganda, hazina makonyo,<br />
mabegu, mpeta na takataka<br />
nyenginezo. Ziwe kavu kwa<br />
kiwango cha kukatika vipande<br />
viwili kwa kutumia vidole na<br />
zenye rangi ya zafarani.<br />
Karafuu zina madini ya Calcium,<br />
Iron, Phosphorus, Sodium,<br />
Potassium, Hydrochloric acid,<br />
na vitamin A na C. Historia<br />
inatwambia kuwa katika karne<br />
ya tatu B.C, China iliweka sheria<br />
kuwa kab<strong>la</strong> ya kuzunguza na<br />
mfalme <strong>la</strong>zima kusafi sha mdomo<br />
kwa kutumia karafuu. Aidha zaidi<br />
ya miaka 2000 iliyopita Wachina<br />
na Wahindi walizitumia karafuu<br />
kama viungo katika vyaku<strong>la</strong>,<br />
dawa ya magonjwa ya meno<br />
na kuondosha harufu mbaya ya<br />
kinywa.<br />
MATUMIZI YA KARAFUU<br />
Madawa<br />
Karafuu ina nguvu za kuponyesha<br />
magonjwa kama ifuatavyo:<br />
• Mafuta ya karafuu yanatumika<br />
katika kuponyesha maumivu<br />
ya meno, vidonda vya ufi zi na<br />
mdomo, hali hii imepelekea<br />
kuingizwa katika dawa za<br />
msuwaki na za kusukutuwa.<br />
Zinc huchanganywa na mafuta<br />
ya karafuu kwa kutibu meno<br />
yenye pango.<br />
`• Mafuta ya karafuu yakipakwa<br />
katika kidonda au mchubuko<br />
huzuwia maradhi ya “fungus”<br />
pia hupunguza maumivu<br />
baada ya kupaka sehemu<br />
ambayo umetafunwa na<br />
wadudu. Ngozi iliyopakwa<br />
mafuta ya karafuu huwa<br />
nyororo na huhifadhika na<br />
magonjwa. Hata hivyo, mafuta<br />
ya karafuu ni makali sana na<br />
yanahitaji kuzimuliwa.<br />
• Mafuta ya karafuu<br />
yanachangamsha na<br />
kuondoa uchovu wa akili na<br />
mwili, upatikanaji usingizi<br />
ikiwa utakunywa kidogo pia<br />
hutumiwa katika kufanya<br />
masaji ambayo huondoa<br />
uchofu wa mwili.<br />
• Mafuta ya karafuu<br />
yakichanganywa na chumvi na<br />
kupakwa kikomoni huondosha<br />
maumivu ya kichwa. Karafuu<br />
zikitafunwa husaidia kusafi sha<br />
koo, kuponya kifua na pumu.<br />
• Mchanganyiko wa mafuta<br />
ya karafuu na mafuta ya<br />
ufuta yakipakwa katika ngozi<br />
huponya magonjwa ya upele.<br />
• Mafuta ya karafuu yanasaidia<br />
kusafi sha damu, kuengeza<br />
7<br />
mzunguko wa damu na<br />
kuengeza kinga ya mwiili.<br />
• Mafuta na karafuu zinatibu<br />
maradhi ya tumbo.<br />
Vipodozi, sabuni na mafuta<br />
mazuri.<br />
• Mafuta ya karafuu (creams )<br />
na mafuta ya kupaka (lotions)<br />
hu<strong>la</strong>inisha ngozi na kuwa<br />
nyororo.<br />
• Mafuta ya karafuu pia<br />
yanatumika katika<br />
kutengeneza mafuta mazuri.<br />
Sigara<br />
Karafuu zinachanganywa na<br />
tumbaku na kutengenezwa sigara<br />
zenye <strong>la</strong>dha nzuri ya karafuu.<br />
Chaku<strong>la</strong><br />
Karafuu inatumika kuongeza<br />
<strong>la</strong>dha katika vyaku<strong>la</strong> kama pi<strong>la</strong>u,<br />
uji, keki, “pudding” na “sausage”.<br />
Unga wa karafuu unachanganjwa<br />
pamoja na unga wa viungo<br />
vyengine kutengeneza masa<strong>la</strong>.<br />
Karafuu zinahitaji kuanikwa katika maeneo yaliyosafi ili kuepuka<br />
kuchanganyika na takataka kwa lengo <strong>la</strong> kupata gredi iliyo bora
Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong> MATUKIO KA<br />
Matukio ka<br />
Raisi wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza <strong>la</strong> Mapinduzi, Mhe. Dkt. Mohamed Ali Shein<br />
akitia saini katika kitabu cha wageni baada ya kuzinduwa uvunaji wa mbegu ya mpunga aina<br />
ya NERICA katika Kituo cha Uzalishaji wa mbegu, Bambi.<br />
Wakulima hujifunza zaidi mbinu bora za uzalishaji wa mazao wanapopata fursa za kushiriki<br />
katika ziara za kimafunzo ambapo hupata wasaa wa kudadisi pamoja na kubadilishana<br />
uzoefu walionao wao wenyewe katika kuendeleza kilimo.<br />
8<br />
Wakulima wa mpunga wa bonde <strong>la</strong> Mtwango n<br />
ya zana za kisasa ikiwemo matrekta madogo<br />
uburugaji wa mashamba ya mpunga.<br />
Upandaji wa mikoko katika maeneo ya pwani<br />
mazingira ya pwani yaliyoharibiwa kutokana n<br />
tatizo <strong>la</strong> kuharibika fukwe na kupanda maji katik
TIKA PICHA Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />
tika Picha<br />
a Bumbwisudi wako mbele katika matumizi<br />
(Power tiller) katika kazi za uchimbuaji na<br />
ni njia moja wapo ya kutunza na kudhibiti<br />
a ukataji ovyo wa mikoko ili kukabiliana na<br />
a maeneo ya kilimo..<br />
Wafanyakazi wa Kitengo cha Utibabu wa Mimea wakiwa katika kazi za kuweka dawa ya<br />
kunasia nzi wa matunda katika mitego maalum ili kukabiliana na tatizo hilo ambalo linarudisha<br />
nyuma juhudi na maendeleo ya wakulima katika kukuza zao <strong>la</strong> matunda.<br />
Wizara ya <strong>Kilimo</strong> na Maliasili katika juhudi zake za kukuza kilimo cha umwagiliaji maji inaendelea<br />
kujenga miundombinu ya umwagiliaji maji kama ilivyoainishwa katika Mpango Mkuu wa Taifa wa<br />
<strong>Kilimo</strong> cha Umwagiliaji maji kwa lengo <strong>la</strong> kwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji na tija.<br />
9
Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong> MABARAZA YA WAKULIMA<br />
MABARAZA YA WAKULIMA NI CHACHU YA<br />
MAENDELEO YA KILIMO ZANZIBAR<br />
Na Shauri Haji<br />
Mabaraza ya wakulima (Farmers<br />
Fora) yaliyoanzishwa miaka minne<br />
iliyopita katika wi<strong>la</strong>ya tisa za Unguja na<br />
Pemba na Programu za Kuimarisha<br />
Huduma za <strong>Kilimo</strong> na Maendeleo ya<br />
Mifugo (ASSP na ASDP-L) Zanzibar ni<br />
vyombo muhimu vya kuwaunganisha<br />
wakulima ingawa dhana hii ni ngeni<br />
katika visiwa hivi.<br />
Mabaraza hayo ya wakulima<br />
yameanzishwa katika Wi<strong>la</strong>ya ya<br />
Magharibi, Kati, Kusini, Kaskazini A na<br />
Kaskazini B, kwa upande wa Unguja na<br />
Wi<strong>la</strong>ya ya Mkoani, Chake chake, Wete<br />
na Micheweni kwa Pemba.<br />
Mabaraza hayo licha ya kuwa na<br />
changangamoto za kiutendaji tangu<br />
yaanzishwe, yamekuwa ni chachu<br />
kwa maendeleo ya kilimo na mifugo<br />
sambamba na kuwa na sauti ya<br />
kumtetea mkulima. Hata hivyo, bado<br />
kuna dhana kwamba programu za<br />
ASSP na ASDP-L ndizo zenye jukumu <strong>la</strong><br />
kugharamia ma baraza hayo.<br />
Dhana ya kuanzishwa kwa Mabaraza ya<br />
Wakulima imekuja baada ya kuona ipo<br />
haja kwa wakulima kuwa na chombo<br />
chao cha kuwaunganisha ili waweze<br />
kutatua matatizo yao kwa pamoja,<br />
kuzijua haki zao na kuzitetea. Tangu<br />
kuanzishwa kwa mabaraza hayo<br />
wakulima wameweza kutatua migogoro<br />
yao ya ardhi hasa katika maeneo yaliyo<br />
nje ya utekelezaji wa miradi ya ASSP na<br />
ASDP-L.<br />
Katibu wa Baraza <strong>la</strong> wakulima <strong>la</strong><br />
Wi<strong>la</strong>ya ya Kati Unguja Bi Mashavu<br />
Juma Mapuri ambae pia ni katibu<br />
wa skuli ya wakulima (FFS) ya Mwera<br />
Kichaka Mabuzi, alisema kwamba<br />
wakulima katika shehia mbali mbali<br />
wanaamini kuwa hiki ni chombo pekee<br />
kinachotumika kupata taarifa na ushauri<br />
kuhusu maendeleo ya uzalishaji wa<br />
mazao ya kilimo na mifugo, kuwatetea,<br />
kuwasemea na kushawishi kuhusu<br />
haki zao na kuwa na sauti ya pamoja ya<br />
kufi kisha maoni na matatizo yao bi<strong>la</strong><br />
woga kwa wahusika.<br />
Alifahamisha juhudi kubwa zilichukuliwa<br />
kuwashajiisha wakulima kutoka shehia<br />
nyengine kujiunga na chombo hicho<br />
na kuondoa dhana potofu miongoni<br />
mwa wakulima kwamba Mabaraza hayo<br />
ni kwa ajili ya shehia zinazotekeleza<br />
miradi iliyo chini ya programu za ASSP<br />
na ASDP-L na kwamba wakulima wa<br />
Waziri wa <strong>Kilimo</strong> na Maliasili Mhe. Mansor Yussuf Himid aliyesimama akiwa<br />
anasisitiza mshikamano wa wakulima wakati akizungumza na wajumbe wa<br />
Mabaraza ya Wakulima huko Dunga Wi<strong>la</strong>ya ya Kati, Unguja.<br />
shehia nyengine hawahusiki. Hali<br />
hiyo imewajengea imani wakulima na<br />
kuweza kufuatilia kwa karibu taarifa<br />
katika Mabaraza ya Wakulima.<br />
Mabaraza hayo yaliundwa kwa<br />
lengo <strong>la</strong> kujenga mashirikiano ya<br />
karibu na watoa huduma binafsi na<br />
kuwajengea uwezo wakulima kitaaluma<br />
na kuwawezesha kuongeza uzalishaji<br />
wenye tija na kupunguza umasikini na<br />
kuongeza kipato. Mabaraza haya kwa<br />
kawaida huwa na wanachama 20<br />
akiwemo Mwenyekiti, Katibu na Mshika<br />
fedha pamoja na wajumbe 17 kwa ki<strong>la</strong><br />
baraza <strong>la</strong> Wi<strong>la</strong>ya.<br />
Miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana<br />
ni pamoja na kuwatembeza wakulima<br />
50 wa muhogo na mazao mengine<br />
katika kikundi cha “Nguvu Kazi<br />
Tusizembee” cha Kisongoni wi<strong>la</strong>ya ya<br />
Kaskazini ‘A’ kinachojishughulisha na<br />
ukulima wa mpunga ambapo wakulima<br />
hao walipata maelezo, kuhamasika<br />
na kuanzisha kilimo cha mpunga<br />
katika maeneo yao. Hayo yalielezwa<br />
na Mwenyekiti wa Baraza <strong>la</strong> Wakulima<br />
<strong>la</strong> Wi<strong>la</strong>ya ya Kaskazini A nd. Abeid Ussi<br />
Haji.<br />
Waziri wa <strong>Kilimo</strong> na Maliasili,<br />
Zanzibar Mhe, Mansoor Yussuf Himid<br />
10<br />
akizungumza na Baraza <strong>la</strong> Wakulima<br />
<strong>la</strong> Wi<strong>la</strong>ya ya Kati, Dunga amekuwa<br />
na imani kubwa na Mabaraza hayo<br />
yaliyoanzishwa Unguja na Pemba.<br />
Aidha, aliwaeleza wakulima Serikali ya<br />
awamu ya saba inayoongozwa na Mhe.<br />
Dk. Ali Mohamed Shein imekusudia<br />
kuleta mageuzi makubwa katika kilimo<br />
kwa kupunguza gharama za pembejeo<br />
muhimu kwa asilimia 75% zikiwemo<br />
mbolea, mbegu, madawa, gharama za<br />
kuchimba na kuburuga ili kumwezesha<br />
mkulima kumudu gharama hizo.<br />
Waziri amelihakikishia baraza <strong>la</strong><br />
wakulima kwamba Wizara yake<br />
inakusudia kuimarisha miundombinu<br />
ya masoko, kuongeza thamani ya<br />
mazao ya kilimo na kujenga barabara<br />
ndogo zinazoingia mashambani kwa<br />
kuziunganisha na barabara kuu ili<br />
kurahisisha usafi rishaji wa mazao ya<br />
wakulima.<br />
Aidha, aliwahakikishia wakulima kuwa<br />
mbegu mpya ya mpunga aina ya<br />
NERICA inayoota katika maeneo ya<br />
juu itazalishwa na kusambazwa kwao<br />
ili waweze kuzalisha zaidi. Wastani<br />
wa tani 140 za NERICA zinatarajiwa<br />
kuzalishwa ili ki<strong>la</strong> mkulima aweze<br />
kutumia mbegu bora kutoka asilimia<br />
zero hadi kufi ka asilimia 33.6.
ATHARI YA JOTO Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />
ATHARI YA JOTO KWA MIFUGO<br />
Na Nassor S. Mohammed<br />
Hali ya hewa inajumuisha ujoto,<br />
unyevu wa hewa, mvua, upepo,<br />
miale ya jua, uzito wa hewa pamoja<br />
na mazingira yote katika maeneo<br />
husika. Kwa kawaida hali ya ujoto<br />
na mvua huwezesha mimea na<br />
mifugo kuishi na kukua vizuri.<br />
Mifugo ni miongoni mwa viumbe<br />
ambavyo hutegemea sana<br />
hali ya hewa katika kuishi na<br />
kuzalisha mazao kama maziwa,<br />
nyama, mayai, manyoya na ngozi<br />
ambavyo hutumiwa kwa chaku<strong>la</strong>,<br />
kutengeneza makoti ya baridi,<br />
mikanda, mikoba na masofa.<br />
Wanyama hawa wanahitaji<br />
hali ya hewa ambayo ni nzuri<br />
kwa ajili ya kuishi na kuzalisha<br />
pindi ikikosekana athari zake<br />
hujitokeza.<br />
Kwa kawaida wanyama wakubwa<br />
wanahitaji joto lenye nyuzi joto kati<br />
ya 37 - 40 sentigredi na wadogo<br />
wanahitaji joto <strong>la</strong> mwili kati ya nyuzi<br />
joto 40- 44 sentigredi, mfano:<br />
Ng’ombe...............38.5 0 C<br />
Kondoo.................38.0 0 C– 39.5 0 C<br />
Kuku wa mayai wanahitaji joto <strong>la</strong> wastani ili waweze ku<strong>la</strong> na kunywa maji kwa<br />
wingi, hali ambayo huchangia zaidi katika utagaji wa mayai.<br />
Mbuzi....................40 0 C<br />
Farasi....................38 0 C<br />
Mbwa....................39 0 C<br />
Paka......................38.5 0 C<br />
Sungura................39.3 0 C<br />
Kuku......................42.1 0 C<br />
Bata.......................21 0 C<br />
Mifugo kama ng’ombe hukuwa vizuri zaidi na kutoa maziwa kwa wingi ikiwa<br />
itawekwa katika maeneo ambayo yana kivuli na kupitisha hewa ya kutosha.<br />
11<br />
Mifugo inapokuwa na joto jingi<br />
katika miili yao, mara nyingi hutoa<br />
jasho na mwili hupoteza joto hilo na<br />
akihisi baridi huzuia utoaji wa jasho<br />
na ujoto hubaki mwilini.<br />
Malisho<br />
Hali ya hewa huchangia katika<br />
uimarikaji wa malisho, u<strong>la</strong>ji na<br />
ukuaji wa mifugo. Mifugo kama<br />
ng’ombe, mbuzi na kondoo<br />
wanapokuwa machungani<br />
ikiwa hali ya hewa ni ya joto kali<br />
hushindwa kutembea na kujitafutia<br />
chaku<strong>la</strong> pia malisho huwa hafi fu.<br />
Hivyo mifugo hukosa chaku<strong>la</strong> cha<br />
kutosha na kushiba. Ng’ombe wa<br />
kienyeji wanaweza kustahamili hali<br />
ya joto ukilinganisha na ng’ombe<br />
wa makabi<strong>la</strong> ya nchi za baridi au<br />
machotara.<br />
Hali ya ubaridi huimarisha malisho<br />
na huiwezesha mifugo kutumia<br />
muda mwingi machungani kujipatia<br />
chaku<strong>la</strong> zaidi bada<strong>la</strong> ya kukaa<br />
kivulini. Ng’ombe na mbuzi wa<br />
kabi<strong>la</strong> za kigeni, mfano Friesian,
Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong> ATHARI ZA JOTO<br />
Jersey na Saanen, Norwegian na<br />
machotara huhitaji chaku<strong>la</strong> kingi<br />
zaidi wakikosa huathirika.<br />
Katika nchi za joto kuna vipindi vya<br />
mvua nyingi ambapo mimea hukua<br />
haraka na kupea mara moja. Kwa<br />
kawaida mifugo hu<strong>la</strong> kidogo sana<br />
majani yaliyokomaa hata kama<br />
itakuwa na njaa kwa sababu majani<br />
hayo yana desturi ya kutoa joto jingi<br />
yanaposagwa mwilini hivyo, joto<br />
jingi husababisha mifugo kutoweza<br />
ku<strong>la</strong> vizuri chaku<strong>la</strong> hicho kwa<br />
manufaa ya miili yao na uzalishaji.<br />
Vyaku<strong>la</strong> vya ziada<br />
Mbali na majani, vyaku<strong>la</strong><br />
vyengine vya ziada kama vile<br />
mabaki ya vyaku<strong>la</strong> vilivyoliwa na<br />
binadamu, maganda ya muhogo,<br />
viazi, magomba, masalia ya<br />
mashambani, pumba, mashudu<br />
na madini yanahitajika kulishia<br />
wanyama. Vyaku<strong>la</strong> hivi ambavyo<br />
hupunguza na havitoi joto jingi<br />
mwilini ni vizuri kupewa wanyama<br />
hasa mifugo ya kabi<strong>la</strong> za nchi za<br />
baridi na machotara ambao kwa<br />
kawaida wanahitaji chaku<strong>la</strong> kingi.<br />
Vyaku<strong>la</strong> vya mifugo vinatakiwa<br />
viweze kupoza joto <strong>la</strong> mwili yaani<br />
vyenye protini. Ng’ombe huacha<br />
ku<strong>la</strong> kabisa wakati mwili wake<br />
ukiwa na joto kali.<br />
Maji<br />
Maji ni muhimu sana katika ukuaji<br />
na uzalishaji wa mifugo na mazao<br />
yake hivyo mifugo inahitaji maji kwa<br />
sababu kuu mbili:<br />
Maji ni chaku<strong>la</strong> na ni sehemu ya<br />
mwili wao. Maji hupoza joto <strong>la</strong> mwili<br />
linalotokana na usagaji na matumizi<br />
ya chaku<strong>la</strong> katika kiwiliwili.<br />
Joto linafanya mifugo inywe maji<br />
mengi, kwa ng’ombe wa kigeni wa<br />
maziwa mwili ufi kapo nyuzi joto<br />
29.4 sentigredi unywaji wa maji<br />
hupungua na kusababisha u<strong>la</strong>ji wa<br />
chaku<strong>la</strong> kuwa mdogo hivyo kuathiri<br />
uzalishaji.<br />
Mifugo iliyozoea maeneo na<br />
mazingira yake hunywa maji kidogo<br />
ukilinganisha na ile ambayo ni<br />
wageni katika eneo hilo mfano<br />
kutoka kwenye baridi kuja kwenye<br />
joto na mvuke mwingi hewani<br />
huifanya mifugo inywe maji mara<br />
kwa mara.<br />
Utoaji wa maziwa<br />
Joto kali husababisha uzalishaji wa<br />
maziwa kuwa mdogo na kuharibika<br />
kirahisi. Ng’ombe wa kigeni<br />
kama Jersey na Friesian wanatoa<br />
maziwa mengi katika mazingira ya<br />
baridi <strong>la</strong>kini joto likizidi njuzijoto<br />
10 sentigredi ng’ombe hawa<br />
hupunguza maziwa na ifi kapo<br />
nyuzijoto 21 hadi 27 sentigredi,<br />
utoaji wa maziwa hushuka kwa<br />
kiwango kikubwa.<br />
Uzazi<br />
Joto, unyevu wa hewani na<br />
mwangaza unachangia katika<br />
kiwango cha uzalishaji wa mifugo.<br />
Joto jingi mwilini linaharibu<br />
mbegu za uzazi za kike na za<br />
kiume pamoja na mayai ambayo<br />
yamepandishiwa yakiwemo katika<br />
harakati za kufanya mtoto. Vizazi<br />
12<br />
vinavyozaliwa nyakati za joto kali<br />
na kutohifadhiwa katika mazingira<br />
mazuri hufa kwa urahisi. Aidha,<br />
joto kali linapunguza utagaji wa<br />
mayai kwa jamii ya kuku.<br />
Maradhi<br />
Hali ya joto inachangia kuishi,<br />
kukua na kuzalisha vimelea na<br />
viumbe vinavyosababisha maradhi<br />
kwa mifugo. Mifugo ya makabi<strong>la</strong><br />
ya kigeni huathiriwa kirahisi na<br />
kupata maradhi. Mazingira mazuri,<br />
shibe na maji husababisha mifugo<br />
kukua haraka, kuwa na afya nzuri<br />
na kuweza kuhimili maradhi.<br />
Mazao ya mifugo<br />
Mazao mengi ya mifugo, mfano<br />
maziwa, nyama na mayai huharibika<br />
haraka yakiwekwa katika hali<br />
ya joto. Ndugu wafugaji inafaa<br />
kuchukua tahadhari ya kutunza<br />
mazao hayo katika maeneo yenye<br />
baridi, pia tunaombwa tutayarishe<br />
malisho kwa ajili ya wakati wa<br />
kiangazi ili wanyama wetu wapate<br />
malisho bora na kuongeza<br />
uzalishaji.<br />
Mbuzi wa maziwa pia wanahitaji mabanda yaliyoinuka, yenye kupitisha hewa na<br />
mwanga wa kutosha ili waweze kukua vizuri na kutoa maziwa kwa wingi.
UJASIRIAMALI Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />
MBINU BORA ZA UJASIRIAMALI<br />
Na Haji A. Omar<br />
Ujasiriamali ni uwezo wa kumudu<br />
na kuendesha biashara kwa<br />
faida katika mazingira ya ushindani<br />
sokoni, uhaba wa mtaji na bi<strong>la</strong> ya<br />
kujali hasara nyengine.<br />
Mjasiriamali ni nani?<br />
Ni mtu ambaye ana maono<br />
ya biashara, mwenye uwezo<br />
wa kugundua fursa, mwenye<br />
msukumo wa kukusanya rasilimali<br />
na kuthubutu kuanzisha mradi kwa<br />
imani kwamba atafanikiwa katika<br />
biashara yake.<br />
Sifa kuu za Mjasiriamali:<br />
• Mwenye kutafuta fursa<br />
• Anaetimiza makubaliano<br />
katika biashara<br />
• Mwenye utashi wa ubora na<br />
ufanisi katika kazi yake<br />
• Mwenye malengo ya muda<br />
mfupi na muda mrefu<br />
• Mwenye uwezo wa kupanga<br />
na kusimamia kazi yake<br />
• Mwenye ari ya kutafuta<br />
habari<br />
• Mwenye uwezo wa<br />
kushawishi na kutoa<br />
ushirikiano<br />
• Anaejiamini na kutenda<br />
Ijapokuwa watu wengi husema<br />
kwamba uwezo wa kijasiriamali ni<br />
kipaji cha kuzaliwa na huthubutu<br />
kufananisha na baadhi ya makabi<strong>la</strong><br />
yanayofanikiwa kibiashara kama<br />
vile, Wakikuyu-Kenya, Wahindi na<br />
Waarabu-Asia, Wachaga-Tanzania<br />
Bara na Wapemba-Zanzibar. Watu<br />
wengine husema Ujasiriamali<br />
unapatikana kwa kusomea, Je nani<br />
yuko sahihi kati ya wenye hoja mbili<br />
hizi?<br />
Utafi ti uliofanywa sehemu tofauti<br />
duniani haukubaliani na hoja ya<br />
kwanza pekee, kuwa mjasiriamali<br />
hamilikiwi na kundi fu<strong>la</strong>ni pekee<br />
Mjasiriamali anaweza kuekeza katika biashara yoyote ile bi<strong>la</strong> ya kujali kutokea kwa<br />
hasara, kinu cha kusagia nafaka ni moja ya biashara hizo.<br />
katika jamii bali mjasiriamali<br />
anaweza kutoka katika kabi<strong>la</strong><br />
na jamii yoyote duniani. Vile vile<br />
wata<strong>la</strong>mu wengi wanakubaliana<br />
kwamba Mjasiriamali akiwa na<br />
sifa zote mbili ndio muama<strong>la</strong> zaidi<br />
kuliko kuwa na kipaji cha kuzaliwa<br />
pekee.<br />
Ki<strong>la</strong> mtu anaweza kuwa mjasiriamali,<br />
cha muhimu ni kuamua, kujituma<br />
na kutenda. Baadhi ya wataa<strong>la</strong>mu<br />
wanasema hakuna mtu anaezaliwa<br />
mjasiriamali, bali watu wengi huiga<br />
au kujifunza ujasiriamali kutoka<br />
kwa waliowazunguka kama vile<br />
wazazi, walezi au kupitia mafunzo<br />
ya fani hiyo. Kwa mantiki hiyo,<br />
yeyote anaweza kuwa mjasiriamali<br />
na mwenye mafanikio makubwa ya<br />
kupigiwa mfano.<br />
USIMAMIZI NA UENDESHAJI WA<br />
BIASHARA ZA KILIMO<br />
Biashara za kilimo<br />
Zinajumuisha utaratibu mzima wa<br />
kupangilia matumizi ya pembejeo<br />
za kilimo ili kuweza kudhibiti na<br />
kutambua uhusiano baina ya<br />
13<br />
pembejeo zilizotumika na mazao<br />
yaliyopatikana katika kipindi<br />
cha uzalishaji. Utaratibu huu<br />
unahusiana na kuelewa uchumi<br />
wa kilimo na mbinu za ujasiriamali<br />
katika kumudu na kuendesha<br />
miradi midogo na mikubwa.<br />
Usimamizi na uendeshaji<br />
Ni utendaji wa kazi kwa kutumia<br />
mtu au kikundi cha watu pamoja<br />
na rasilimali nyingine kwa utaratibu<br />
maalum uliopangwa ili kuweza<br />
kufi kia malengo yaliyokusudiwa.<br />
Kazi za usimamizi na uendeshaji<br />
ni pamoja na kupanga, kuongoza,<br />
kuhamasisha, kuajiri, kudhibiti na<br />
kutathmini.<br />
Mambo muhimu ili msimamizi<br />
aweze kufanya kazi zake vizuri:<br />
• Awe mwenye kuielewa kazi<br />
yake vizuri<br />
• Atoe au kupata motisha<br />
• Afuate taratibu za sheria<br />
• Awe mwenye kufahamu<br />
mazingira ya kazi<br />
• Awe na uwezo wa kufanya
Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong> UJASIRIAMALI<br />
tathmini ya kazi<br />
Sifa za mjasiriamali katika<br />
kusimamia biashara:<br />
1. Kuweka malengo kwa<br />
usahihi na yawe mahsusi,<br />
yanayopimika, yanayofi kika,<br />
yanayofaa na yanayoweza<br />
kufuatiliwa.<br />
2. Kuwa na mfumo wa taarifa na<br />
kuweka kumbukumbu kama<br />
vile kudhibiti na kutathmini<br />
maendeleo, kufanya maamuzi<br />
na kupanga mipango ijayo,<br />
kuelewa mbinu mpya juu<br />
ya teknolojia, masoko na<br />
mazingira.<br />
3. Muda ni bidhaa muhimu kuliko<br />
bidhaa nyengine na kama<br />
muda hautunzwi hakutakua<br />
na maendeleo mazuri. Muda<br />
ni kigezo kikuu cha utendaji<br />
ukitunzwa huleta ufanisi.<br />
Kutunza muda ni kugawa muda<br />
huo kwa ajili ya kuweka malengo<br />
kwa umuhimu wake, kugundua<br />
na kuondosha vipoteza muda na<br />
kutumia maarifa ya uongozi ili<br />
kufi kia malengo kiufanisi zaidi.<br />
Mambo ya kuzingatia:<br />
• Hakuna namna ya kuweza<br />
kufi dia muda – Dakika<br />
moja iliyopotea haiwezi<br />
kurudi tena<br />
• Panga mambo yako kwa<br />
vipaumbele ili kuokoa<br />
muda<br />
• Hakuna muda mchache,<br />
kuona muda mchache ni<br />
dalili za uongozi mbaya<br />
• Ku<strong>la</strong><strong>la</strong> wakati wa usiku ni<br />
njia pekee ya kupumzika na<br />
sio kucheza gemu au kukaa<br />
maskani wakati wa mchana<br />
kama ndio njia muafaka ya<br />
kupumzika<br />
Mambo yafuatayo husababisha mtu<br />
kupoteza muda bi<strong>la</strong> kujijua au kwa<br />
kujua kwa maana ya kupumzika:<br />
• Kucheza gemu na kuandika<br />
ujumbe wa maandishi sana<br />
katika simu<br />
• Kupokea na kufurahia<br />
wageni wanaokuja bi<strong>la</strong><br />
miadi<br />
• Kutoweka malengo na<br />
vipaumbele vya kazi<br />
• Kucheza karata, draft na<br />
bao <strong>la</strong> kete wakati wa kazi<br />
• Dawati lililojaa karatasi bi<strong>la</strong><br />
mpango<br />
• Kutogawa kazi kikamilifu<br />
au kufanya kazi zinazoweza<br />
kufanywa na walio chini<br />
yako<br />
• Kufanya mambo mengi kwa<br />
wakati mmoja<br />
• Kushindwa kusema hapana<br />
au siwezi<br />
• Ukosefu wa nidhamu<br />
4. Motisha ni kitu chochote<br />
kinachohimiza juhudi katika<br />
kazi. Kwa kawaida binaadamu<br />
akipata motisha huongeza<br />
juhudi. Vifuatavyo ni vitu<br />
vitolewavyo ili kuongeza juhudi:<br />
• Motisha kwa wafanyakazi<br />
ni kama vile kumpandisha<br />
cheo, kupata bonasi<br />
yanapotokea mafanikio<br />
makubwa na ongezeko <strong>la</strong><br />
mshahara<br />
• Motisha kwa wateja ni<br />
kama vile kupunguza bei,<br />
usafi ri wa bure, nyongeza<br />
ya kitu juu ya bidhaa<br />
aliyonunua, huduma<br />
nzuri kwa mteja ukiwemo<br />
14<br />
ukarimu na uchangamfu.<br />
5. Mawasiliano kwa mjasiriamali<br />
ni njia pekee ya kupokea<br />
habari kwa haraka, husaidia<br />
wateja kuelewa huduma,<br />
biashara au bidhaa zitolewazo<br />
na kupokea maoni ya wateja.<br />
Usipoitangaza biashara yako na<br />
kutafuta taarifa itakua vigumu<br />
kuingia katika ulimwengu wa<br />
biashara, kama vile usemi<br />
maarufu usemavyo “BIASHARA<br />
ITANGAZWAYO NDIO ITOKAYO”<br />
Zipo njia tofauti za mawasiliano<br />
zinazotumiwa na wajasiriamali.<br />
Miongoni mwake ni :<br />
• Mawasiliano kwa<br />
maandishi kama vile<br />
mabango ya matangazo,<br />
barua, vipeperushi, ripoti,<br />
lebo za kwenye bidhaa<br />
humuwezesha mjasiriamali<br />
kuwasiliana na wateja<br />
wake au wadau wengine<br />
wa biashara.<br />
• Mawasiliano kwa njia ya<br />
maongezi kupitia mijada<strong>la</strong>,<br />
warsha, kongamano,<br />
semina na mikutano.<br />
Mjasiriamali anaweza<br />
kupata muda mzuri wa<br />
kuwasiliana na wateja kwa<br />
kushiriki kwenye mafunzo<br />
ya shamba darasa, sehemu<br />
za maonyesho ya bidhaa<br />
kama vile maonesho ya<br />
biashara na ya wakulima<br />
• Mawasiliano ya ishara kama<br />
vile ishara za uso, mikono,<br />
mabega na kichwa, njia<br />
hii hutumika kwa wateja<br />
au wadau wengine wa<br />
biashara mara nyingi njia<br />
hii hutoa ujumbe mzuri au<br />
mbaya. Hivyo mjasiriamali<br />
<strong>la</strong>zima awe makini na<br />
ishara atoazo mteja hata<br />
kama wateja wanawasiliana<br />
wao wenyewe wanapokuwa<br />
katika eneo <strong>la</strong> biashara.
RASILIMALI ZA MSITUNI Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />
UMUHIMU WA RASILIMALI ZA MSITUNI<br />
Na Nassor S. Mkarafuu<br />
Rasilimali za msituni zina uasili<br />
wa kibaiolojia zikijumuisha<br />
wanyama na mimea ya aina na<br />
rika tofauti yenye faida kwa maisha<br />
ya viumbe pamoja na huduma<br />
zinazopatikana msituni au ardhi<br />
inayotumika. Kuwepo kwa rasilimali<br />
hizi kunategemea uwepo wa msitu.<br />
Rasilimali za msituni zina faida<br />
nyingi kwa maisha ya viumbe<br />
wakiwemo binadamu, wanyama<br />
na wadudu. Miongoni mwa faida<br />
za moja kwa moja ni upatikanaji<br />
wa chaku<strong>la</strong>, miti ya mapambo,<br />
vichanganyisho vya manukato,<br />
mbegu pamoja na upatikanaji wa<br />
wanyama na mimea yenye kutoa<br />
tiba.<br />
Faida nyengine ni pamoja na<br />
uhifadhi wa vyanzo vya maji,<br />
kurekebisha hali ya hewa, ufyonzaji<br />
wa hewa mkaa, uhifadhi wa udongo<br />
na kuzuia mmong’onyoko, ambapo<br />
katika nchi nyingi za Afrika,<br />
rasilimali hizi zina umuhimu wa<br />
upatikanaji wa lishe kwa kaya.<br />
UTEGEMEZI WA JAMII KWA<br />
MAZAO YAPATIKANAYO MSITUNI<br />
Duniani kote jamii zinategemea<br />
rasilimali zinazopatikana msituni<br />
ikiwemo kujikimu kwa chaku<strong>la</strong>,<br />
malisho ya wanyama, madawa na<br />
zana za ujenzi. Matumizi mengine<br />
ni pamoja na kupatikana zana<br />
za ukulima, utengenezaji wa<br />
mapambo ya majumbani.<br />
Nchi nyingi za Afrika na Asia,<br />
jamii hutegemea rasilimali hizo<br />
kwa kuongeza kipato cha kaya,<br />
kupata uhakika wa chaku<strong>la</strong> na<br />
lishe, biashara na ajira kwa<br />
ujum<strong>la</strong>. Hata hivyo rasilimali hizo<br />
hazipewi umuhimu na wanasiasa<br />
na wapangaji wa mipango ya<br />
Maendeleo licha ya umuhimu wake,<br />
mara nyingi watu hutoa thamani<br />
ya msitu pale tu yanapopatikana<br />
mavuno yake, kuyatumia,<br />
kutengeneza bidhaa, kuziuza na<br />
kuchangia kuoengeza kipato kwa<br />
jamii za vijijini. Rasilimali hizi ni<br />
kiashirio kikubwa katika kupunguza<br />
Misitu huchangia katika upatikanaji wa rasilimali nyingi pamoja na umuhimu<br />
wake husaidia katika kuhifadhi mazingira na vyanzo vya maji.<br />
umasikini kwa jamii zinazotegemea<br />
msitu kwa kuongeza kipato, kupata<br />
uhakika wa chaku<strong>la</strong>.<br />
Uhakika wa Chaku<strong>la</strong> na Lishe<br />
Rasilimali za msituni zina mchango<br />
mkubwa katika kuchangia uhakika<br />
wa chaku<strong>la</strong> na lishe katika jamii<br />
kwa nyanja tofauti kama vile<br />
kupata chaku<strong>la</strong> kinachochangia<br />
kutoa vitamini, madini, uanga<br />
na protini muhimu. Jamii nyingi<br />
za vijjini zinatumia vyaku<strong>la</strong><br />
vinavyopatikana msituni kwa ku<strong>la</strong><br />
au kuuza kwa lengo <strong>la</strong> kupata pesa<br />
za kununulia chaku<strong>la</strong> hasa wakati<br />
wa uhaba wa mavuno ya mazao<br />
mashambani. Miongoni mwa<br />
mazao yanayopatikana msituni<br />
ni pamoja na matunda, mboga<br />
mboga, wanyama pori na asali.<br />
Matunda<br />
Mabungo, Zambarau, Fuu, Ukwaju,<br />
Ubuyu, Mapera, Pilipilidoria, Maviru,<br />
Kunazi na Chongoma. Aidha, katika<br />
baadhi ya nchi za Afrika mazao<br />
kama edible nuts zinatumika kwa<br />
chaku<strong>la</strong>, mafuta ya ku<strong>la</strong>, viungo,<br />
achari na vinywaji.<br />
Mbogamboga<br />
15<br />
Miongoni mwa mboga<br />
zinazopatikana ni kikwayakwaya,<br />
pwipwi, mchicha mwiba, mchunga,<br />
mronge, mchambale, mboga ya<br />
pwani na mnavu. Aina hizi za mboga<br />
za asili zinatoa madini mengi zaidi<br />
kuliko aina ya mboga zisizokuwa za<br />
asili. Inasemekana mboga za asili<br />
zina madini ya chokaa (calcium)<br />
1.5 – 3.2 zaidi ya mboga mboga za<br />
jamii ya kabeji ambazo ndizo zenye<br />
madini ya chokaa (calcium) nyingi<br />
kwa mboga zisizokuwa za asili.<br />
Wanyama pori<br />
Wanyama pori ni miongoni mwa<br />
chaku<strong>la</strong> muhimu katika kuongeza<br />
uhakika wa chaku<strong>la</strong> na lishe<br />
wakijumuisha wanyama, ndege<br />
na mayai yao pamoja na samaki.<br />
Nyama itokanayo na wanyama<br />
hawa ni chanzo cha protini na<br />
madini mengine kama chuma,<br />
vitamin A na B. Wanyama wadogo<br />
(paa) na ndege (kanga) ni maarufu<br />
katika kuongeza chaku<strong>la</strong> na lishe<br />
ya jamii.<br />
Asali<br />
Ni miongoni mwa chaku<strong>la</strong> maarufu<br />
hapa nchini. Kawaida asali iliyo<br />
nyingi hutengenezwa na nyuki<br />
na hupatikana msituni baada ya
Toleo <strong>la</strong> Saba<br />
Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />
kuvunwa ambayo hutumika katika<br />
jamii kwa ku<strong>la</strong>, dawa na biashara.<br />
miongoni na Faida nyengine,<br />
masega ya nyuki hutumika katika<br />
kutengeneza mshumaa na maji<br />
maji yaitwayo royal jelly.<br />
Matumizi ya asali yanatofautiana<br />
kutoka sehemu moja hadi nyengine<br />
kutokana na upatikanaji na hali<br />
ya soko. Wananchi wa vijijini mara<br />
nyingi hutumia asali kama dawa ya<br />
kutibu maradhi mbali mbali pamoja<br />
na kuuza kwa kujiongezea kipato.<br />
Hapa Zanzibar lita moja inauzwa<br />
kwa wastani wa shilingi 12, 000.<br />
Hii inamaanisha kwamba asali<br />
ni moja kati ya rasilimali yenye<br />
umuhimu katika afya na kuongeza<br />
kipato katika jamii.<br />
Dawa za asili<br />
Dawa za asili ni mazao muhimu<br />
yanayopatikana kutoka msituni<br />
ambapo nchi zote za Afrika<br />
zinatumika. Zaidi ya watu bilioni<br />
3.5 wanaoishi pembezoni mwa<br />
misitu duniani wanatumia dawa<br />
za asili na inakisiwa aina 35,000<br />
zinatumika ambapo katika nchi<br />
za Afrika zaidi ya asilimia 80 ya<br />
watu wanatumia dawa za asili kwa<br />
matibabu ya maradhi na maumivu<br />
mbali mbali. Shirika <strong>la</strong> Afya Duniani<br />
(WHO) limekisia kwamba zaidi ya<br />
asilimia 80 ya watu katika nchi<br />
zinazoendelea wanategemea dawa<br />
za asili kwa matibabu ya msingi na<br />
zinapatikana kwa urahisi na jamii<br />
inazifahamu.<br />
Miongoni mwa miti ya dawa<br />
maarufu zinazotumika hapa nchini<br />
ni pamoja na Mchofu, Mvuje,<br />
Mtarawanda, Kivumbasi, Mwavikali<br />
na Mpande ambazo zinatumika<br />
kwa kutibu maradhi mbali mbali<br />
kwa binadamu yakiwemo maradhi<br />
ya tumbo, kichwa, ngiri pamoja<br />
Kima punju ni miongoni mwa rasilimali ya msituni ambayo ni kivutio kikuu cha<br />
Msitu wa Hifadhi wa Jozani kwa watalii wa ndani na wa nje ya nchi.<br />
na maradhi ya matumbo ya<br />
kinamama.<br />
Miti ya mapambo<br />
Miti hii inatumika maalumu kwa<br />
ajili ya mapambo katika maeneo<br />
inayoishi jamii na kupendezesha<br />
hali ya mandhari. Jamii nyingi<br />
zinatumia miti hii katika nyumba<br />
zao au katika sehemu ambazo watu<br />
hupenda kupumzika na kwenye<br />
mahoteli za kitalii. Miongoni mwa<br />
miti maarufu inayotumika kwa<br />
mapambo inayopatikana msituni<br />
ni pamoja na Mgwede, Mkonge,<br />
Mkuyu na Mnunu ambayo pamoja<br />
na kutumika kwa mapambo pia<br />
hutumika kwa kutoa kivuli.<br />
Uhifadhi wa vyanzo vya maji<br />
Maji ni rasilimali za misitu<br />
zinazosaidia uzalishaji wa bidhaa<br />
mbali mbali na kuongeza pato <strong>la</strong><br />
taifa na yanasaidia kwa afya ya<br />
binaadamu. Maji ya mito, maziwa,<br />
mvua na sehemu za unyevu ni<br />
vyanzo muhimu vya uzalishaji wa<br />
mazao. Misitu inasaidia kuhifadhi<br />
kina cha maji, kupatika kwa<br />
uhakika na kupunguza chumvi<br />
katika maji. Aidha, miti inatoa nafasi<br />
ya makaazi ya samaki. Majani<br />
na magogo yalioza yanaongeza<br />
virutubisho kwa viumbe waishio<br />
majini.<br />
Rasilimali zinazopatikana msituni<br />
ni muhimu na zinahitaji kuwekewa<br />
mkakati maalum wa kuziendeleza<br />
na kuzitunza kwa vile zinachangia<br />
kustawisha uchumi wa nchi kwa<br />
kuongeza pato <strong>la</strong> taifa na usitawi<br />
wa maisha ya mwanadamu pamoja<br />
na viumbe vyengine. Aidha, taasisi<br />
zinazohusika ni vyema kufanya<br />
utafi ti na kuweza kuzitangaza<br />
rasilimali hizi na kuzianisha kwa<br />
jamii na matumizi yake.<br />
GAZETI HILI HUTOLEWA KILA BAADA YA MIEZI MITATU NA<br />
WIZARA YA KILIMO NA MALIASILI - ZANZIBAR<br />
P. O. Box 159 Zanzibar, Simu: +255 24 2230986, Fax: +255 24 2234650<br />
Barua pepe: kilimo@zanlink.com, Tovuti: www.kilimoznz.or.tz