12.12.2012 Views

Jarida la Kilimo, Julai - Septemba, 2011

Jarida la Kilimo, Julai - Septemba, 2011

Jarida la Kilimo, Julai - Septemba, 2011

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Toleo <strong>la</strong> Saba<br />

ISSN: 1821-8113 Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza <strong>la</strong> Mapinduzi Mhe: Dkt. Ali Mohamed Shein wa pili<br />

kutoka kushoto pomoja na viongozi wengine akiwa katika harakati za uvunaji wa mpunga wa<br />

mbegu aina ya NERICA kituo cha uzalishaji wa mbegu Bambi, Wi<strong>la</strong>ya ya Kati Unguja.<br />

Yaliyomo<br />

Maoni ya Mhariri/Picha ya Ja<strong>la</strong>da...........................................................................Uk.2<br />

Uvunaji na Uanikaji wa Karafuu............................................................................Uk.3 - 4<br />

Upotevu wa Rutuba na Urutubishaji wa Ardhi.......................................................Uk.4 - 5<br />

Uvunaji na Uanikaji wa Karafuu..............................................................................Uk.6 - 7<br />

Matukio katika Picha.............................................................................................Uk.8 - 9<br />

Mabaraza ya Wakulima..........................................................................................Uk.10<br />

Athari za Joto kwa Mifugo...............................................................................Uk.11 - 12<br />

Mbinu Bora za Ujasiriamali..............................................................................Uk.13 - 14<br />

Umuhimu wa Rasilimali za Msituni......................................................................Uk. 15 - 16


Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong> WAHARIRI/MAONI/PICHA YA JARIDA<br />

Bodi ya Wahariri MAONI YA MHARIRI<br />

Washauri<br />

Affan O. Maalim<br />

Juma Ali Juma<br />

Dk. Bakar S. Asseid<br />

Mhariri Mkuu<br />

Dk. Juma M. Akil<br />

Msanifu na Mhariri<br />

Mtendaji<br />

Hashim H. Chande<br />

Wahariri Wasaidizi<br />

Makame M. Abdulrahman<br />

Nassor S. Mkarafuu<br />

Nassor S. Mohammed<br />

Mpiga chapa<br />

Fatma A. Juma<br />

Mpiga picha<br />

Khamis A. Bakari<br />

ANUWANI<br />

Wizara ya <strong>Kilimo</strong>,<br />

Maliasili - Zanzibar<br />

S.L.P. 159<br />

Simu: +255 24 2230986<br />

Fax: +255 24 2234650<br />

E-mail: kilimo@zanlink.com<br />

Tovuti: kilimoznz.or.tz<br />

Ndugu wakulima, kupata chaku<strong>la</strong> cha kutosha na kilicho<br />

bora kwa ki<strong>la</strong> mwananchi ni sua<strong>la</strong> gumu ambalo linahitaji<br />

mipango na mikakati mizuri ya serikali kupitia Wizara<br />

husika. Moja ya tatizo kubwa linalowakabili wananchi ni<br />

kuchelewa kukamilisha hatua za mwanzo za matayarisho ya<br />

mashamba, kulima eneo kubwa ambalo hawana uwezo nalo<br />

na kutokutumia zana na pembejeo bora za kilimo.<br />

Ndugu wakulima, moja ya kikwazo kikubwa ni uwezo mdogo<br />

wa kutumia zana bora za kilimo, mbegu bora, mbolea na<br />

kutozingatia kanuni na taaluma bora za uzalishaji ambazo<br />

zinatolewa na Wizara ya <strong>Kilimo</strong> na Maliasili. Vikwazo hivi<br />

humsababishia mkulima kutumia nguvu nyingi, muda<br />

mrefu na kupata mavuno hafi fu na tija ndogo.<br />

Ndugu wakulima, kwa miaka mingi neno “Ukulima wa<br />

Kisasa” limekuwa ni wimbo <strong>la</strong>kini bado mkulima wa visiwani<br />

anategemea zana na pembejeo duni kama vile mbegu na<br />

jembe <strong>la</strong> mkono (kijembe kongoroka). Serikali ya Mapinduzi<br />

ya Zanzibar kupitia Wizara ya <strong>Kilimo</strong> na Maliasili inafanya<br />

mabadiliko makubwa katika kilimo ili kukifanya kilimo hicho<br />

kiwe katika mfumo wa kisasa “Mapinduzi ya <strong>Kilimo</strong>”.<br />

Ndugu wakulima, katika kufanikisha sua<strong>la</strong> hili Serikali<br />

imeongeza upatikanaji wa pembejeo na zana za kilimo<br />

yakiwemo matrekta makubwa na madogo, mbegu bora na<br />

mbolea, kuongeza usamabazaji wa taaluma kwa wakulima<br />

kwa kuongeza idadi ya mabwana/mabibishamba katika<br />

shehia pamoja na kutoa ruzuku ya aslimia 75% kwa kazi za<br />

utayarishaji wa mashamba na ununuzi wa mbegu bora na<br />

mbolea.<br />

Ndugu wakulima, hatunabudi kuunga mkono juhudi hizi<br />

za Serikali ili kufanikisha azma ya “Mapinduzi ya <strong>Kilimo</strong>”<br />

hivyo tunaipongeza na tunaiomba iendelee na juhudi zake<br />

za kuwashajiisha na kuwashirikisha wakulima kikamilifu<br />

katika kupanga malengo yao juu ya mpango wa utumiaji wa<br />

zana na pembejeo bora za kilimo.<br />

Ndugu wakulima, kwa kuunga mkono juhudi hizi za Serikali,<br />

Wizara ya <strong>Kilimo</strong> na Maliasili itaendelea kutoa mafunzo ya<br />

utumiaji bora wa zana na pembejeo za kilimo na kuweka<br />

mpango maalumu ya mafunzo kwa ki<strong>la</strong> shehia juu ya<br />

umuhimu wa zana hizo pamoja na matumizi yake ili kufi kia<br />

lengo <strong>la</strong> wakulima katika kujitosheleza kwa chaku<strong>la</strong>, kuinua<br />

hali zao za maisha na kuipunguzia mzigo Serikali wa kuagiza<br />

chaku<strong>la</strong> kutoka nje ya nchi.<br />

PICHA YA JALADA<br />

Katika picha anaonekana Rais wa Zanzibar Mhe. Ali Mohamed Shein<br />

akivuna mpunga wa mbegu aina ya NERICA katika shamba <strong>la</strong> kuzalisha<br />

mbegu liliopo Bambi pamoja nae kutoka kulia kwake ni Waziri wa<br />

<strong>Kilimo</strong> na Maliasili Mhe, Mansoor Y. Himid, Mkuu wa Mkoa wa Kusini<br />

(U) Mhe, Mustafa Ibrahim na Naibu Katibu Mkuu (kilimo) ndugu Juma<br />

A. Juma, tarehe 7 Ju<strong>la</strong>i <strong>2011</strong>.<br />

2


MAZAO BORA Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />

ILI TUVUNE MAZAO BORA NI LAZIMA TUPANDE<br />

MBEGU BORA ZINAZOWEZA KUTUPATIA TIJA<br />

Na Sabiha H. Saleh<br />

Mnamo tarehe 2/7/<strong>2011</strong> Rais<br />

wa Zanzibar na Mwenyekiti wa<br />

Baraza <strong>la</strong> mapinduzi Mhe. Dkt. Ali<br />

Mohammed Shein aliyasema hayo<br />

kwa nyakati tofauti aliposhiriki<br />

kikamilifu katika uzinduzi wa Kitaifa<br />

wa uvunaji wa mbegu ya mpunga aina<br />

ya “NERICA”, huko Bambi na bonde<br />

<strong>la</strong> Kisima Mchanga liliopo Kiboje<br />

Mkwajuni Wi<strong>la</strong>ya ya Kati Unguja.<br />

Hii ni hatua mojawapo ya Serikali ya<br />

mapinduzi ya Zanzibar katika jitihada<br />

zake za kukuza na kuendeleza kilimo<br />

kwa ujum<strong>la</strong>.<br />

Dkt. Shein amesema kuwa lengo kuu<br />

<strong>la</strong> Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar<br />

kufanya mapinduzi ya kilimo tayari<br />

limeanza kutekelezwa na mbegu<br />

aina ya NERICA ndio mkombozi wetu<br />

kwani Serikali itaendelea kuchukua<br />

ki<strong>la</strong> jitihada kuona kuwa wakulima wa<br />

Zanzibar wananufaika na kilimo chao<br />

pamoja na taifa kwa ujum<strong>la</strong>.<br />

Alisema kuwa azma ya Serikali kwa<br />

upande wake ni kuona kuwa Mapinduzi<br />

ya kilimo yanaleta tija kwa wakulima<br />

pamoja na wananchi kwa ujum<strong>la</strong> kwa<br />

kuweza kupata kile kilichokusudiwa.<br />

Aidha, amefahamisha kuwa nia na<br />

dhamira ni kuwainua wakulima na<br />

Serikali inaendelea na taratibu za<br />

kuwaletea wakulima wake mashine<br />

za kuvunia mpunga, kuwapunguzia<br />

bei za pembejeo pamoja na kuwapatia<br />

matrekta kwa ajili ya kuvurugia na<br />

dawa za kuulia wadudu ili mkulima<br />

aweze kumudu gharama za uendeshaji<br />

na tuweze kulima kwa tija zaidi.<br />

Akizungumzia kuhusiana na mfumko<br />

wa bei za vyaku<strong>la</strong> hasa mchele ambao<br />

ndio chaku<strong>la</strong> kikubwa kwa watu wa<br />

Zanzibar amesema kuwa Serikali tayari<br />

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza <strong>la</strong> Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed<br />

Shein aliyesimama na shuke <strong>la</strong> mpunga akiwa katika uzinduzi wa uvunaji wa mbegu<br />

ya mpunga aina ya NERICA katika Shamba <strong>la</strong> Uzalishaji wa mbegu Bambi<br />

imeshaanza kutekeleza mapinduzi ya<br />

kilimo kwa kupambana na hali hiyo.<br />

Akifafanua zaidi kuhusu ongezeko <strong>la</strong><br />

Idadi ya Watu duniani, kwa upande wa<br />

Zanzibar amesema tokea Mapinduzi<br />

Matukufu ya Januari mwaka 1964<br />

ambapo idadi ya watu ilikuwa 320,000<br />

hadi mwaka 1974 ilikuwa ni 640,000<br />

na kwa mujibu wa takwimu ya sensa<br />

ya mwaka 2002 ambapo ilifi kia watu<br />

milioni 1.2 idadi ambayo inapelekea<br />

ongezeko <strong>la</strong> mahitaji ya chaku<strong>la</strong>.<br />

Kutokana na ongezeko <strong>la</strong> watu ,<br />

takwimu zinaonyesha kwamba mchele<br />

unaotumiwa kwa chaku<strong>la</strong> hapa<br />

Zanzibar ni tani 80,000 kwa mwaka,<br />

unaozalishwa na wakulima ni chini ya<br />

tani 16,000 na kiasi chote kilichobaki<br />

hununuliwa kutoka nje ya nchi. Aidha,<br />

Dkt. Shein alisisitiza haja ya kuongeza<br />

uzalishaji wa chaku<strong>la</strong>.<br />

Pia aliwataka wakulima kufuata<br />

ushauri wa wata<strong>la</strong>mu na kubadilika ili<br />

kilimo chetu kiwe cha kisasa. Hivyo,<br />

hatuna budi kutumia teknolojia ya<br />

3<br />

kisasa na kuweza kujitegemea katika<br />

kilimo cha mpunga kwa anga<strong>la</strong>u<br />

asilimia 60, “Ukitumia mbegu bora<br />

unaweza kuvuna mavuno bora”.<br />

Amefahamisha kuwa kulima kwa<br />

kutumia mbegu bora kunapelekea<br />

kuvuna mazao mengi na bora, hivyo<br />

tuongeze jitihada na kukifanya chaku<strong>la</strong><br />

kuongezeka.<br />

Aidha Dkt. Shein amesema kuwa<br />

Washirika wa Maendeleo wako tayari<br />

na wanaendelea na jitihada za kuiunga<br />

mkono Zanzibar katika Sekta ya <strong>Kilimo</strong><br />

wakiwemo, Korea ya Kusini, Marekani,<br />

Japan hasa katika mradi wao wa ‘Feed<br />

the Future’.<br />

Akiwa katika bonde <strong>la</strong> Kisima<br />

Mchanga, Dkt. Shein aliwaahidi<br />

wakulima kuwajengea njia yao kwa<br />

kiwango cha kifusi kutoka barabara<br />

kuu hadi bondeni, kuwawekea umeme,<br />

kuwachimbia kisima na kuwapatia<br />

tre<strong>la</strong> <strong>la</strong> kubebea mizigo.<br />

Akimkaribisha Rais wa Zanzibar


Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong> UPOTEVU WA RUTUBA NA URUTUBISHAJI ARDHI<br />

Waziri wa <strong>Kilimo</strong> na Maliasili Mhe.<br />

Mansoor Yussuf Himid amesema kuwa<br />

Mapinduzi ya <strong>Kilimo</strong> ni mageuzi ya<br />

haraka yalioendelevu katika kukipa<br />

nguvu zaidi kilimo pamoja na wakulima<br />

kwani faida inayopatikana huwa ni kwa<br />

taifa zima.<br />

Amefahamisha kuwa hali ya Ulimwengu<br />

imebadilika na sisi <strong>la</strong>zi tubadilike tuwe<br />

na mikakati imara katika kukibadilisha<br />

kilimo chetu kwa faida ya nchi yetu.<br />

Alisema kuwa dhamira ya Wizara ya<br />

<strong>Kilimo</strong> na Maliasili ndani ya miaka<br />

mitano ni kulima hekta 6,000 za<br />

umwagijiliaji maji, kati ya hekta<br />

8,521 ambapo kwa sasa ni hekta<br />

700 tu ndizo zinazolimwa. Aidha,<br />

alifahamisha kuwa Jamhuri ya Korea<br />

ya Kusini imeahidi kusaidia kulima<br />

hekta 2,000 na Serikali ya Marekani<br />

hekta 2,000.<br />

Aliongeza kusema kuwa mashamba<br />

UPOTEVU WA RUTUBA NA NJIA<br />

ZA KURUTUBISHA ARDHI<br />

Na Hashim H. Chande<br />

Ardhi yenye rutuba ni muhimu<br />

katika ukuwaji wa mimea na<br />

upatikanaji wa mavuno yaliyo bora.<br />

Kama tunavyoelewa kuwa rutuba<br />

ni chaku<strong>la</strong> cha mimea ambacho<br />

kinapatikana kwenye udongo. Ili<br />

kuuweka udongo katika hali ya<br />

rutuba na kuiwezesha mimea<br />

iendelee kukua vizuri ardhini hatuna<br />

budi kutumia mbolea ili kurudisha<br />

chaku<strong>la</strong> kilichochukuliwa na mimea.<br />

Mbolea zinatumika kuongeza<br />

rutuba na kuiwezesha ardhi kutoa<br />

mazao mengi, kinachohitajika ni<br />

jinsi ya kujua aina gani ya mbolea,<br />

kiwango, na wakati zinapohitajika.<br />

Hivyo Mabwana/mabibi shamba<br />

waliomo katika maeneo ya kilimo<br />

wanajukumu <strong>la</strong> kuwaelimisha<br />

wakulima wa sehemu hizo.<br />

Tishio <strong>la</strong> upoteaji wa rutuba<br />

darasa yataongezwa hadi kufi kia<br />

1,200, pia mashamba darasa manne<br />

ya mikarafuu yataanzishwa, mawili<br />

Unguja na mawili Pemba.<br />

Mhe. Waziri wa <strong>Kilimo</strong> aliwaeleza<br />

wakulima kuwa katika bajeti ya Wizara<br />

ya mwaka <strong>2011</strong>/2012 itakuwa na<br />

matumaini kwa wakulima wa visiwa<br />

hivi.<br />

Nae Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja<br />

Mhe. Mustafa Muhammed Ibrahim<br />

aliwatoa hofu wakulima wa bonde<br />

<strong>la</strong> Kisimamchanga na kuwataka<br />

kuendelea kulitumia bonde hilo kwani<br />

tayari limeshapimwa na Wizara ya<br />

<strong>Kilimo</strong> kwa lengo <strong>la</strong> kuanza kilimo cha<br />

umwagiliaji maji.<br />

Nao wakulima wa bonde <strong>la</strong><br />

Kisimamchanga wameushukuru mradi<br />

wa PADEP uliotumia zaidi ya shilingi<br />

milioni 32 ambao umeleta mafanikio<br />

makubwa kwa kuongeza uzalishaji<br />

Ardhi iliyopoteza rutuba imeshambuliwa na ukame na hutoa mazao hafi fu au kutoweza<br />

kutoa mazao ya aina yoyote.<br />

4<br />

kutoka polo 4 kwa robo hekta kwa<br />

sasa, wakati hapo zamani walikuwa<br />

wakizalisha polo 4 kwa hekta nzima.<br />

Jum<strong>la</strong> ya hekta 5 za mbegu ya mpunga<br />

wa aina ya ‘NERICA’ zimevunwa na<br />

zinatarajiwa kupandwa kwa wingi<br />

katika msimu wa mvua za vuli zijazo<br />

kwa lengo <strong>la</strong> kupandwa wakati wa<br />

masika ambapo zinatarajiwa zaidi ya<br />

tani 3,700 kupatikana katika msimu<br />

ujao wa masika ili kufi kia asilimia 50%<br />

ya uzalishaji ndani ya miaka mitano.<br />

Uzinduzi huo wa kitaifa uliwashirikisha<br />

viongozi kutoka Mikoa 5 ya Unguja<br />

na Pemba, wakiwemo Mawaziri,<br />

Wawakilishi, Mkuu wa Mkoa wa Kusini<br />

ambaye ndiye mwenyeji wa shughuli<br />

hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mjini/<br />

Magharibi, Mkuu wa Mkoa wa Kusini<br />

Pemba, Viongozi wa Serikali pamoja<br />

na Wakisiasa na wananchi kutoka<br />

maeneo mbalimbali.


UPOTEVU WA RUTUBA NA URUTUBISHAJI ARDHI Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />

Mchanganyiko wa vitu tofauti vilivyotumika katika kutengenezea mboji ikiwemo<br />

majani, udongo, takataka, mabaki ya mimea na maji.<br />

katika udongo<br />

Katika nchi yetu tumekabiliwa na<br />

tishio kubwa <strong>la</strong> kupoteza rutuba<br />

ya udongo kutokana uharibifu wa<br />

mazingira unaosababishwa na<br />

ukataji wa miti ovyo, kuchimba<br />

mchanga, kuchimba na kukata<br />

matofali ya mawe na kilimo<br />

kisichozingatia kanuni bora.<br />

Ardhi inayotumiwa vibaya kwa kilimo<br />

pasi na kurudishia rutuba yake<br />

ni chanzo kikubwa cha upotevu<br />

wa rutuba hiyo ya asili ambayo ni<br />

chaku<strong>la</strong> muhimu cha mimea na<br />

viumbe vyengine vinavyoishi katika<br />

udongo. Upungufu huo husababisha<br />

udongo kupunguza uwezo wake wa<br />

kuhifadhi maji kwa muda mrefu<br />

ambapo ukame hutokea na mazao<br />

yanayopandwa kutoa mavuno<br />

hafi fu.<br />

Rutuba hiyo ni <strong>la</strong>zima irudishwe<br />

ili tuweze kupata tena mavuno<br />

bora. Hivyo, tunapaswa kuzingatia<br />

urutubishaji wa ardhi kwa kuweka<br />

viwango sahihi vya mbolea<br />

kulingana na mahitaji halisi ya<br />

mimea iliyopandwa, kwa mfano<br />

mpunga unahitaji kiasi cha kilo 100 -<br />

150 cha mbolea kwa ki<strong>la</strong> ekari mbili<br />

na nusu (2.5). Kwa wale wakulima<br />

wenye tabia ya kupumzisha ardhi<br />

kwa kipindi cha mwaka mmoja au<br />

miwili kwa kuchunga wanyama au<br />

kuweka mazizi katika maeneo hayo<br />

wakati wa kupumzisha ardhi, njia hii<br />

husaidia kurudisha rutuba ardhini<br />

ijapokuwa hivi sasa haitumiki sana<br />

katika maeneo mengi kutokana<br />

na ongezeko kubwa <strong>la</strong> mahitaji ya<br />

ardhi.<br />

Kutokana na ongezeko <strong>la</strong> mahitaji ya<br />

matumizi ya mbolea za viwandani na<br />

gharama kubwa za upatikanaji wake,<br />

wakulima hatuna budi kujitengezea<br />

mbolea sisi wenyewe kwa kutumia<br />

malighafi tulizonazo kama vile<br />

kupanda mazao ya jamii ya kunde,<br />

matumizi mboji na samadi.<br />

UTENGENEZAJI WA MBOLEA YA<br />

MBOJI<br />

Ili kudumisha uzalishaji wa chaku<strong>la</strong>,<br />

wakulima wa Zanzibar wanasisitizwa<br />

kutengeneza na kutumia mbolea<br />

ya samadi, mboji na takataka pale<br />

ambapo zinapopatikana kwa urahisi.<br />

Mbolea hizi mbali ya kurutubisha<br />

ardhi, pia husaidia kuifanya ardhi<br />

iwe katika hali nzuri iliyoshikamana.<br />

Ingawa wakulima wanahimizwa<br />

kutumia mbolea za viwandani kwa<br />

baadhi ya mazao, <strong>la</strong>kini sirahisi<br />

kufi dia pengo <strong>la</strong> mbolea yote<br />

inayohitajika kwa wakati huu ambao<br />

ardhi inaonyesha kuchoka, kutokana<br />

na matumizi mabaya ya mfululizo.<br />

Kupuuza mbolea hizi kunaweza<br />

kuleta madhara makubwa katika<br />

kilimo.<br />

5<br />

Mbolea ya mboji ni mchanganyiko<br />

wa mabaki ya vitu vyenye asili ya<br />

uhai ambavyo hukusanywa kutoka<br />

mashambani na majumbani kama<br />

vile takataka, mabua ya mimea,<br />

magugu, vinyesi vya wanyama au<br />

hata mbolea ya chumvi chumvi.<br />

FAIDA YA MBOLEA YA MBOJI<br />

• Hukaa ardhini na hutumiwa na<br />

mimea kwa muda mrefu, kuliko<br />

mbolea ya chumvi.<br />

• Mboji ina uwezo wa kubadili hali<br />

ya udongo na kuufanya utumike<br />

kwa kilimo.<br />

• Mboji inawezesha udongo<br />

kuhifadhi unyevu kwa muda<br />

mrefu.<br />

• Mboji ni rahisi kutengeneza,<br />

kutumiwa na haina gharama<br />

kubwa ukilinganisha na mbolea<br />

za viwandani.<br />

JINSI YA KUTENGENEZA<br />

i Safi sha eneo unalotaka<br />

kutengeneza mbolea.<br />

ii Pima mita 1.5 urefu na mita 1.5<br />

upana na weka fi to baada ya<br />

kupima urefu na upana, urefu<br />

wa fi to unategemea mahitaji ya<br />

mkulima.<br />

iii Chimbua chimbua na weka vizuri<br />

udongo.<br />

iv Panga tabaka <strong>la</strong> udongo, majani,<br />

mabua na kuyatandaza pamoja<br />

na takataka zinazoweza kuoza.<br />

iii Weka tabaka <strong>la</strong> udongo wa<br />

kutosha juu mabua na majani<br />

kwa mpangilio.<br />

iv Tumia mbolea ya chumvi chumvi<br />

au vinyesi vya wanyama kwa<br />

kunyunyizia juu ya udongo.<br />

v Nyunyizia maji baada ya kuweka<br />

mbolea, kwa kumalizia tabaka <strong>la</strong><br />

kwanza. Rudia kuweka tabaka <strong>la</strong><br />

pili mpaka <strong>la</strong> tatu juu yake kwa<br />

kufata mpangilio ule ule wa<br />

tabaka <strong>la</strong> mwanzo hadi kufi kia<br />

urefu wa mita 1-2.<br />

vi Hakikisha tabaka lina unyevu na<br />

joto <strong>la</strong> kutosha. Geuza tabaka<br />

hizo ki<strong>la</strong> baada ya wiki mbili<br />

kwa kupunguza hewa na unyevu<br />

uliozidi ili kuozesha takataka<br />

kikalifu.<br />

vii Mbolea hiyo inatakiwa itumike<br />

baada ya kuoza na kupoa.


Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong> KARAFUU<br />

UVUNAJI NA UANIKAJI KARAFUU<br />

Na Rashid Khamis<br />

Zanzibar imekuwa ikijulikana<br />

sana katika uuzaji wa karafuu<br />

bora kuanzia karne ya 18, karafuu<br />

bora zinapatikana kutoana na<br />

uchumaji, uchambuaji, uanikaji<br />

bora pamoja na usafi shaji wa<br />

karafuu kab<strong>la</strong> ya kuuza. Katika<br />

miaka ya 2000 tumeshuhudia<br />

kurejeshwa kwa uchafu wa<br />

karafuu zilizouzwa nje katika<br />

Shirika <strong>la</strong> Biashara <strong>la</strong> Taifa<br />

<strong>la</strong> Zanzibar (ZSTC) Hali hii<br />

inasababisha Zanzibar kupoteza<br />

sifa yake ya kuuza karafuu bora.<br />

UVUNAJI<br />

Karafuu nzuri kwa biashara<br />

ni yenye rangi kutoka kijani<br />

na kuingia rangi ya manjano<br />

kab<strong>la</strong> ya kuchanua. Karafuu<br />

ikachanua inabadilika na kuwa<br />

mbegu na hupoteza matumizi<br />

yaliyokusudiwa.<br />

Wakati wa uchumaji wa karafuu ni<br />

vizuri kuepuka ukataji wa matawi<br />

kwani tabia hii hudhoofi sha<br />

mikarafuu na husababisha<br />

kushambuliwa na maradhi na<br />

hatimae kufa.<br />

Mwananchi akiwa katika harakati za kuvuna karafuu ili kuliokoa zao hili<br />

<strong>la</strong> kitaifa lisipotee<br />

Wakati wa kuchuma, matawi<br />

dhaifu ya mikarafuu mikubwa<br />

yafungwe pamoja kwa kutumia<br />

kamba. Aidha Hii itasaidia<br />

kufanya yawe madhubuti zaidi,<br />

hivyo kupunguza uwezekano wa<br />

kukwanyuka kutokana na uzito<br />

wa mchumaji. Kamba au vingoe<br />

Mwanamama akiwa mstari wa mbele katika kushiriki kuchambua<br />

karafuu kwa lengo <strong>la</strong> kuliokoa zao hili <strong>la</strong> Taifa<br />

6<br />

vitumike kwa kuvuta matawi<br />

yaliyombali ili yaweze kuchumwa<br />

kirahisi bada<strong>la</strong> ya kuyavunja.<br />

Mikarafuu midogo inaweza<br />

kuchumwa kwa kutumia ngazi na<br />

hii inasaidia kupunguza kwa kiasi<br />

kikubwa uharibifu huo.<br />

UANIKAJI<br />

Karafuu zianikwe haraka baada<br />

ya kuchambuliwa na kusafi shwa<br />

na hakikisha sehemu za kuanikia<br />

zinapata jua wakati wote (kutwa<br />

nzima). Usianike karafuu karibu<br />

na jengo lolote au miti mirefu<br />

inayoweza kutoa kivuli.<br />

Miongoni mwa vifaa vilivyo bora<br />

kwa kuanikia karafuu ni majamvi<br />

kwa sababu huhifadhi karafuu<br />

vizuri zaidi wakati wa mvua<br />

kuliko aina nyengine za vifaa<br />

kama magunia. Magunia yakiroa<br />

hufyonza maji na kurowesha<br />

karafuu, pia hupunguza gredi<br />

kwa kutoa nyuzi ambazo<br />

huchanganyika na karafuu.<br />

Karafuu zinazoanikwa juu ya<br />

sakafu ziendelee kuwekwa kwenye<br />

majamvi kwa vile sakafu huchuna


KARAFUU Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />

karafuu wakati wa kugeuza na<br />

kuanua. Inashauria majamvi<br />

yawekwe juu ya majani mafupi<br />

kuepuka kuingia vumbi. Haitakiwi<br />

kuanika karafuu pembezoni mwa<br />

barabara ili kuepusha kupoteza<br />

ubora wake kwa kuchanganyika<br />

na vitu vengine, kupondwa na gari<br />

au kukanyagwa na wapita njia.<br />

Karafuu bora zinatakiwa ziwe na<br />

sifa zifuatazo:<br />

• Ziwe hazina vitawi, vijiti na<br />

matende nzima na zenye<br />

umbo <strong>la</strong> namna moja<br />

zisizoganda, hazina makonyo,<br />

mabegu, mpeta na takataka<br />

nyenginezo. Ziwe kavu kwa<br />

kiwango cha kukatika vipande<br />

viwili kwa kutumia vidole na<br />

zenye rangi ya zafarani.<br />

Karafuu zina madini ya Calcium,<br />

Iron, Phosphorus, Sodium,<br />

Potassium, Hydrochloric acid,<br />

na vitamin A na C. Historia<br />

inatwambia kuwa katika karne<br />

ya tatu B.C, China iliweka sheria<br />

kuwa kab<strong>la</strong> ya kuzunguza na<br />

mfalme <strong>la</strong>zima kusafi sha mdomo<br />

kwa kutumia karafuu. Aidha zaidi<br />

ya miaka 2000 iliyopita Wachina<br />

na Wahindi walizitumia karafuu<br />

kama viungo katika vyaku<strong>la</strong>,<br />

dawa ya magonjwa ya meno<br />

na kuondosha harufu mbaya ya<br />

kinywa.<br />

MATUMIZI YA KARAFUU<br />

Madawa<br />

Karafuu ina nguvu za kuponyesha<br />

magonjwa kama ifuatavyo:<br />

• Mafuta ya karafuu yanatumika<br />

katika kuponyesha maumivu<br />

ya meno, vidonda vya ufi zi na<br />

mdomo, hali hii imepelekea<br />

kuingizwa katika dawa za<br />

msuwaki na za kusukutuwa.<br />

Zinc huchanganywa na mafuta<br />

ya karafuu kwa kutibu meno<br />

yenye pango.<br />

`• Mafuta ya karafuu yakipakwa<br />

katika kidonda au mchubuko<br />

huzuwia maradhi ya “fungus”<br />

pia hupunguza maumivu<br />

baada ya kupaka sehemu<br />

ambayo umetafunwa na<br />

wadudu. Ngozi iliyopakwa<br />

mafuta ya karafuu huwa<br />

nyororo na huhifadhika na<br />

magonjwa. Hata hivyo, mafuta<br />

ya karafuu ni makali sana na<br />

yanahitaji kuzimuliwa.<br />

• Mafuta ya karafuu<br />

yanachangamsha na<br />

kuondoa uchovu wa akili na<br />

mwili, upatikanaji usingizi<br />

ikiwa utakunywa kidogo pia<br />

hutumiwa katika kufanya<br />

masaji ambayo huondoa<br />

uchofu wa mwili.<br />

• Mafuta ya karafuu<br />

yakichanganywa na chumvi na<br />

kupakwa kikomoni huondosha<br />

maumivu ya kichwa. Karafuu<br />

zikitafunwa husaidia kusafi sha<br />

koo, kuponya kifua na pumu.<br />

• Mchanganyiko wa mafuta<br />

ya karafuu na mafuta ya<br />

ufuta yakipakwa katika ngozi<br />

huponya magonjwa ya upele.<br />

• Mafuta ya karafuu yanasaidia<br />

kusafi sha damu, kuengeza<br />

7<br />

mzunguko wa damu na<br />

kuengeza kinga ya mwiili.<br />

• Mafuta na karafuu zinatibu<br />

maradhi ya tumbo.<br />

Vipodozi, sabuni na mafuta<br />

mazuri.<br />

• Mafuta ya karafuu (creams )<br />

na mafuta ya kupaka (lotions)<br />

hu<strong>la</strong>inisha ngozi na kuwa<br />

nyororo.<br />

• Mafuta ya karafuu pia<br />

yanatumika katika<br />

kutengeneza mafuta mazuri.<br />

Sigara<br />

Karafuu zinachanganywa na<br />

tumbaku na kutengenezwa sigara<br />

zenye <strong>la</strong>dha nzuri ya karafuu.<br />

Chaku<strong>la</strong><br />

Karafuu inatumika kuongeza<br />

<strong>la</strong>dha katika vyaku<strong>la</strong> kama pi<strong>la</strong>u,<br />

uji, keki, “pudding” na “sausage”.<br />

Unga wa karafuu unachanganjwa<br />

pamoja na unga wa viungo<br />

vyengine kutengeneza masa<strong>la</strong>.<br />

Karafuu zinahitaji kuanikwa katika maeneo yaliyosafi ili kuepuka<br />

kuchanganyika na takataka kwa lengo <strong>la</strong> kupata gredi iliyo bora


Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong> MATUKIO KA<br />

Matukio ka<br />

Raisi wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza <strong>la</strong> Mapinduzi, Mhe. Dkt. Mohamed Ali Shein<br />

akitia saini katika kitabu cha wageni baada ya kuzinduwa uvunaji wa mbegu ya mpunga aina<br />

ya NERICA katika Kituo cha Uzalishaji wa mbegu, Bambi.<br />

Wakulima hujifunza zaidi mbinu bora za uzalishaji wa mazao wanapopata fursa za kushiriki<br />

katika ziara za kimafunzo ambapo hupata wasaa wa kudadisi pamoja na kubadilishana<br />

uzoefu walionao wao wenyewe katika kuendeleza kilimo.<br />

8<br />

Wakulima wa mpunga wa bonde <strong>la</strong> Mtwango n<br />

ya zana za kisasa ikiwemo matrekta madogo<br />

uburugaji wa mashamba ya mpunga.<br />

Upandaji wa mikoko katika maeneo ya pwani<br />

mazingira ya pwani yaliyoharibiwa kutokana n<br />

tatizo <strong>la</strong> kuharibika fukwe na kupanda maji katik


TIKA PICHA Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />

tika Picha<br />

a Bumbwisudi wako mbele katika matumizi<br />

(Power tiller) katika kazi za uchimbuaji na<br />

ni njia moja wapo ya kutunza na kudhibiti<br />

a ukataji ovyo wa mikoko ili kukabiliana na<br />

a maeneo ya kilimo..<br />

Wafanyakazi wa Kitengo cha Utibabu wa Mimea wakiwa katika kazi za kuweka dawa ya<br />

kunasia nzi wa matunda katika mitego maalum ili kukabiliana na tatizo hilo ambalo linarudisha<br />

nyuma juhudi na maendeleo ya wakulima katika kukuza zao <strong>la</strong> matunda.<br />

Wizara ya <strong>Kilimo</strong> na Maliasili katika juhudi zake za kukuza kilimo cha umwagiliaji maji inaendelea<br />

kujenga miundombinu ya umwagiliaji maji kama ilivyoainishwa katika Mpango Mkuu wa Taifa wa<br />

<strong>Kilimo</strong> cha Umwagiliaji maji kwa lengo <strong>la</strong> kwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji na tija.<br />

9


Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong> MABARAZA YA WAKULIMA<br />

MABARAZA YA WAKULIMA NI CHACHU YA<br />

MAENDELEO YA KILIMO ZANZIBAR<br />

Na Shauri Haji<br />

Mabaraza ya wakulima (Farmers<br />

Fora) yaliyoanzishwa miaka minne<br />

iliyopita katika wi<strong>la</strong>ya tisa za Unguja na<br />

Pemba na Programu za Kuimarisha<br />

Huduma za <strong>Kilimo</strong> na Maendeleo ya<br />

Mifugo (ASSP na ASDP-L) Zanzibar ni<br />

vyombo muhimu vya kuwaunganisha<br />

wakulima ingawa dhana hii ni ngeni<br />

katika visiwa hivi.<br />

Mabaraza hayo ya wakulima<br />

yameanzishwa katika Wi<strong>la</strong>ya ya<br />

Magharibi, Kati, Kusini, Kaskazini A na<br />

Kaskazini B, kwa upande wa Unguja na<br />

Wi<strong>la</strong>ya ya Mkoani, Chake chake, Wete<br />

na Micheweni kwa Pemba.<br />

Mabaraza hayo licha ya kuwa na<br />

changangamoto za kiutendaji tangu<br />

yaanzishwe, yamekuwa ni chachu<br />

kwa maendeleo ya kilimo na mifugo<br />

sambamba na kuwa na sauti ya<br />

kumtetea mkulima. Hata hivyo, bado<br />

kuna dhana kwamba programu za<br />

ASSP na ASDP-L ndizo zenye jukumu <strong>la</strong><br />

kugharamia ma baraza hayo.<br />

Dhana ya kuanzishwa kwa Mabaraza ya<br />

Wakulima imekuja baada ya kuona ipo<br />

haja kwa wakulima kuwa na chombo<br />

chao cha kuwaunganisha ili waweze<br />

kutatua matatizo yao kwa pamoja,<br />

kuzijua haki zao na kuzitetea. Tangu<br />

kuanzishwa kwa mabaraza hayo<br />

wakulima wameweza kutatua migogoro<br />

yao ya ardhi hasa katika maeneo yaliyo<br />

nje ya utekelezaji wa miradi ya ASSP na<br />

ASDP-L.<br />

Katibu wa Baraza <strong>la</strong> wakulima <strong>la</strong><br />

Wi<strong>la</strong>ya ya Kati Unguja Bi Mashavu<br />

Juma Mapuri ambae pia ni katibu<br />

wa skuli ya wakulima (FFS) ya Mwera<br />

Kichaka Mabuzi, alisema kwamba<br />

wakulima katika shehia mbali mbali<br />

wanaamini kuwa hiki ni chombo pekee<br />

kinachotumika kupata taarifa na ushauri<br />

kuhusu maendeleo ya uzalishaji wa<br />

mazao ya kilimo na mifugo, kuwatetea,<br />

kuwasemea na kushawishi kuhusu<br />

haki zao na kuwa na sauti ya pamoja ya<br />

kufi kisha maoni na matatizo yao bi<strong>la</strong><br />

woga kwa wahusika.<br />

Alifahamisha juhudi kubwa zilichukuliwa<br />

kuwashajiisha wakulima kutoka shehia<br />

nyengine kujiunga na chombo hicho<br />

na kuondoa dhana potofu miongoni<br />

mwa wakulima kwamba Mabaraza hayo<br />

ni kwa ajili ya shehia zinazotekeleza<br />

miradi iliyo chini ya programu za ASSP<br />

na ASDP-L na kwamba wakulima wa<br />

Waziri wa <strong>Kilimo</strong> na Maliasili Mhe. Mansor Yussuf Himid aliyesimama akiwa<br />

anasisitiza mshikamano wa wakulima wakati akizungumza na wajumbe wa<br />

Mabaraza ya Wakulima huko Dunga Wi<strong>la</strong>ya ya Kati, Unguja.<br />

shehia nyengine hawahusiki. Hali<br />

hiyo imewajengea imani wakulima na<br />

kuweza kufuatilia kwa karibu taarifa<br />

katika Mabaraza ya Wakulima.<br />

Mabaraza hayo yaliundwa kwa<br />

lengo <strong>la</strong> kujenga mashirikiano ya<br />

karibu na watoa huduma binafsi na<br />

kuwajengea uwezo wakulima kitaaluma<br />

na kuwawezesha kuongeza uzalishaji<br />

wenye tija na kupunguza umasikini na<br />

kuongeza kipato. Mabaraza haya kwa<br />

kawaida huwa na wanachama 20<br />

akiwemo Mwenyekiti, Katibu na Mshika<br />

fedha pamoja na wajumbe 17 kwa ki<strong>la</strong><br />

baraza <strong>la</strong> Wi<strong>la</strong>ya.<br />

Miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana<br />

ni pamoja na kuwatembeza wakulima<br />

50 wa muhogo na mazao mengine<br />

katika kikundi cha “Nguvu Kazi<br />

Tusizembee” cha Kisongoni wi<strong>la</strong>ya ya<br />

Kaskazini ‘A’ kinachojishughulisha na<br />

ukulima wa mpunga ambapo wakulima<br />

hao walipata maelezo, kuhamasika<br />

na kuanzisha kilimo cha mpunga<br />

katika maeneo yao. Hayo yalielezwa<br />

na Mwenyekiti wa Baraza <strong>la</strong> Wakulima<br />

<strong>la</strong> Wi<strong>la</strong>ya ya Kaskazini A nd. Abeid Ussi<br />

Haji.<br />

Waziri wa <strong>Kilimo</strong> na Maliasili,<br />

Zanzibar Mhe, Mansoor Yussuf Himid<br />

10<br />

akizungumza na Baraza <strong>la</strong> Wakulima<br />

<strong>la</strong> Wi<strong>la</strong>ya ya Kati, Dunga amekuwa<br />

na imani kubwa na Mabaraza hayo<br />

yaliyoanzishwa Unguja na Pemba.<br />

Aidha, aliwaeleza wakulima Serikali ya<br />

awamu ya saba inayoongozwa na Mhe.<br />

Dk. Ali Mohamed Shein imekusudia<br />

kuleta mageuzi makubwa katika kilimo<br />

kwa kupunguza gharama za pembejeo<br />

muhimu kwa asilimia 75% zikiwemo<br />

mbolea, mbegu, madawa, gharama za<br />

kuchimba na kuburuga ili kumwezesha<br />

mkulima kumudu gharama hizo.<br />

Waziri amelihakikishia baraza <strong>la</strong><br />

wakulima kwamba Wizara yake<br />

inakusudia kuimarisha miundombinu<br />

ya masoko, kuongeza thamani ya<br />

mazao ya kilimo na kujenga barabara<br />

ndogo zinazoingia mashambani kwa<br />

kuziunganisha na barabara kuu ili<br />

kurahisisha usafi rishaji wa mazao ya<br />

wakulima.<br />

Aidha, aliwahakikishia wakulima kuwa<br />

mbegu mpya ya mpunga aina ya<br />

NERICA inayoota katika maeneo ya<br />

juu itazalishwa na kusambazwa kwao<br />

ili waweze kuzalisha zaidi. Wastani<br />

wa tani 140 za NERICA zinatarajiwa<br />

kuzalishwa ili ki<strong>la</strong> mkulima aweze<br />

kutumia mbegu bora kutoka asilimia<br />

zero hadi kufi ka asilimia 33.6.


ATHARI YA JOTO Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />

ATHARI YA JOTO KWA MIFUGO<br />

Na Nassor S. Mohammed<br />

Hali ya hewa inajumuisha ujoto,<br />

unyevu wa hewa, mvua, upepo,<br />

miale ya jua, uzito wa hewa pamoja<br />

na mazingira yote katika maeneo<br />

husika. Kwa kawaida hali ya ujoto<br />

na mvua huwezesha mimea na<br />

mifugo kuishi na kukua vizuri.<br />

Mifugo ni miongoni mwa viumbe<br />

ambavyo hutegemea sana<br />

hali ya hewa katika kuishi na<br />

kuzalisha mazao kama maziwa,<br />

nyama, mayai, manyoya na ngozi<br />

ambavyo hutumiwa kwa chaku<strong>la</strong>,<br />

kutengeneza makoti ya baridi,<br />

mikanda, mikoba na masofa.<br />

Wanyama hawa wanahitaji<br />

hali ya hewa ambayo ni nzuri<br />

kwa ajili ya kuishi na kuzalisha<br />

pindi ikikosekana athari zake<br />

hujitokeza.<br />

Kwa kawaida wanyama wakubwa<br />

wanahitaji joto lenye nyuzi joto kati<br />

ya 37 - 40 sentigredi na wadogo<br />

wanahitaji joto <strong>la</strong> mwili kati ya nyuzi<br />

joto 40- 44 sentigredi, mfano:<br />

Ng’ombe...............38.5 0 C<br />

Kondoo.................38.0 0 C– 39.5 0 C<br />

Kuku wa mayai wanahitaji joto <strong>la</strong> wastani ili waweze ku<strong>la</strong> na kunywa maji kwa<br />

wingi, hali ambayo huchangia zaidi katika utagaji wa mayai.<br />

Mbuzi....................40 0 C<br />

Farasi....................38 0 C<br />

Mbwa....................39 0 C<br />

Paka......................38.5 0 C<br />

Sungura................39.3 0 C<br />

Kuku......................42.1 0 C<br />

Bata.......................21 0 C<br />

Mifugo kama ng’ombe hukuwa vizuri zaidi na kutoa maziwa kwa wingi ikiwa<br />

itawekwa katika maeneo ambayo yana kivuli na kupitisha hewa ya kutosha.<br />

11<br />

Mifugo inapokuwa na joto jingi<br />

katika miili yao, mara nyingi hutoa<br />

jasho na mwili hupoteza joto hilo na<br />

akihisi baridi huzuia utoaji wa jasho<br />

na ujoto hubaki mwilini.<br />

Malisho<br />

Hali ya hewa huchangia katika<br />

uimarikaji wa malisho, u<strong>la</strong>ji na<br />

ukuaji wa mifugo. Mifugo kama<br />

ng’ombe, mbuzi na kondoo<br />

wanapokuwa machungani<br />

ikiwa hali ya hewa ni ya joto kali<br />

hushindwa kutembea na kujitafutia<br />

chaku<strong>la</strong> pia malisho huwa hafi fu.<br />

Hivyo mifugo hukosa chaku<strong>la</strong> cha<br />

kutosha na kushiba. Ng’ombe wa<br />

kienyeji wanaweza kustahamili hali<br />

ya joto ukilinganisha na ng’ombe<br />

wa makabi<strong>la</strong> ya nchi za baridi au<br />

machotara.<br />

Hali ya ubaridi huimarisha malisho<br />

na huiwezesha mifugo kutumia<br />

muda mwingi machungani kujipatia<br />

chaku<strong>la</strong> zaidi bada<strong>la</strong> ya kukaa<br />

kivulini. Ng’ombe na mbuzi wa<br />

kabi<strong>la</strong> za kigeni, mfano Friesian,


Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong> ATHARI ZA JOTO<br />

Jersey na Saanen, Norwegian na<br />

machotara huhitaji chaku<strong>la</strong> kingi<br />

zaidi wakikosa huathirika.<br />

Katika nchi za joto kuna vipindi vya<br />

mvua nyingi ambapo mimea hukua<br />

haraka na kupea mara moja. Kwa<br />

kawaida mifugo hu<strong>la</strong> kidogo sana<br />

majani yaliyokomaa hata kama<br />

itakuwa na njaa kwa sababu majani<br />

hayo yana desturi ya kutoa joto jingi<br />

yanaposagwa mwilini hivyo, joto<br />

jingi husababisha mifugo kutoweza<br />

ku<strong>la</strong> vizuri chaku<strong>la</strong> hicho kwa<br />

manufaa ya miili yao na uzalishaji.<br />

Vyaku<strong>la</strong> vya ziada<br />

Mbali na majani, vyaku<strong>la</strong><br />

vyengine vya ziada kama vile<br />

mabaki ya vyaku<strong>la</strong> vilivyoliwa na<br />

binadamu, maganda ya muhogo,<br />

viazi, magomba, masalia ya<br />

mashambani, pumba, mashudu<br />

na madini yanahitajika kulishia<br />

wanyama. Vyaku<strong>la</strong> hivi ambavyo<br />

hupunguza na havitoi joto jingi<br />

mwilini ni vizuri kupewa wanyama<br />

hasa mifugo ya kabi<strong>la</strong> za nchi za<br />

baridi na machotara ambao kwa<br />

kawaida wanahitaji chaku<strong>la</strong> kingi.<br />

Vyaku<strong>la</strong> vya mifugo vinatakiwa<br />

viweze kupoza joto <strong>la</strong> mwili yaani<br />

vyenye protini. Ng’ombe huacha<br />

ku<strong>la</strong> kabisa wakati mwili wake<br />

ukiwa na joto kali.<br />

Maji<br />

Maji ni muhimu sana katika ukuaji<br />

na uzalishaji wa mifugo na mazao<br />

yake hivyo mifugo inahitaji maji kwa<br />

sababu kuu mbili:<br />

Maji ni chaku<strong>la</strong> na ni sehemu ya<br />

mwili wao. Maji hupoza joto <strong>la</strong> mwili<br />

linalotokana na usagaji na matumizi<br />

ya chaku<strong>la</strong> katika kiwiliwili.<br />

Joto linafanya mifugo inywe maji<br />

mengi, kwa ng’ombe wa kigeni wa<br />

maziwa mwili ufi kapo nyuzi joto<br />

29.4 sentigredi unywaji wa maji<br />

hupungua na kusababisha u<strong>la</strong>ji wa<br />

chaku<strong>la</strong> kuwa mdogo hivyo kuathiri<br />

uzalishaji.<br />

Mifugo iliyozoea maeneo na<br />

mazingira yake hunywa maji kidogo<br />

ukilinganisha na ile ambayo ni<br />

wageni katika eneo hilo mfano<br />

kutoka kwenye baridi kuja kwenye<br />

joto na mvuke mwingi hewani<br />

huifanya mifugo inywe maji mara<br />

kwa mara.<br />

Utoaji wa maziwa<br />

Joto kali husababisha uzalishaji wa<br />

maziwa kuwa mdogo na kuharibika<br />

kirahisi. Ng’ombe wa kigeni<br />

kama Jersey na Friesian wanatoa<br />

maziwa mengi katika mazingira ya<br />

baridi <strong>la</strong>kini joto likizidi njuzijoto<br />

10 sentigredi ng’ombe hawa<br />

hupunguza maziwa na ifi kapo<br />

nyuzijoto 21 hadi 27 sentigredi,<br />

utoaji wa maziwa hushuka kwa<br />

kiwango kikubwa.<br />

Uzazi<br />

Joto, unyevu wa hewani na<br />

mwangaza unachangia katika<br />

kiwango cha uzalishaji wa mifugo.<br />

Joto jingi mwilini linaharibu<br />

mbegu za uzazi za kike na za<br />

kiume pamoja na mayai ambayo<br />

yamepandishiwa yakiwemo katika<br />

harakati za kufanya mtoto. Vizazi<br />

12<br />

vinavyozaliwa nyakati za joto kali<br />

na kutohifadhiwa katika mazingira<br />

mazuri hufa kwa urahisi. Aidha,<br />

joto kali linapunguza utagaji wa<br />

mayai kwa jamii ya kuku.<br />

Maradhi<br />

Hali ya joto inachangia kuishi,<br />

kukua na kuzalisha vimelea na<br />

viumbe vinavyosababisha maradhi<br />

kwa mifugo. Mifugo ya makabi<strong>la</strong><br />

ya kigeni huathiriwa kirahisi na<br />

kupata maradhi. Mazingira mazuri,<br />

shibe na maji husababisha mifugo<br />

kukua haraka, kuwa na afya nzuri<br />

na kuweza kuhimili maradhi.<br />

Mazao ya mifugo<br />

Mazao mengi ya mifugo, mfano<br />

maziwa, nyama na mayai huharibika<br />

haraka yakiwekwa katika hali<br />

ya joto. Ndugu wafugaji inafaa<br />

kuchukua tahadhari ya kutunza<br />

mazao hayo katika maeneo yenye<br />

baridi, pia tunaombwa tutayarishe<br />

malisho kwa ajili ya wakati wa<br />

kiangazi ili wanyama wetu wapate<br />

malisho bora na kuongeza<br />

uzalishaji.<br />

Mbuzi wa maziwa pia wanahitaji mabanda yaliyoinuka, yenye kupitisha hewa na<br />

mwanga wa kutosha ili waweze kukua vizuri na kutoa maziwa kwa wingi.


UJASIRIAMALI Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />

MBINU BORA ZA UJASIRIAMALI<br />

Na Haji A. Omar<br />

Ujasiriamali ni uwezo wa kumudu<br />

na kuendesha biashara kwa<br />

faida katika mazingira ya ushindani<br />

sokoni, uhaba wa mtaji na bi<strong>la</strong> ya<br />

kujali hasara nyengine.<br />

Mjasiriamali ni nani?<br />

Ni mtu ambaye ana maono<br />

ya biashara, mwenye uwezo<br />

wa kugundua fursa, mwenye<br />

msukumo wa kukusanya rasilimali<br />

na kuthubutu kuanzisha mradi kwa<br />

imani kwamba atafanikiwa katika<br />

biashara yake.<br />

Sifa kuu za Mjasiriamali:<br />

• Mwenye kutafuta fursa<br />

• Anaetimiza makubaliano<br />

katika biashara<br />

• Mwenye utashi wa ubora na<br />

ufanisi katika kazi yake<br />

• Mwenye malengo ya muda<br />

mfupi na muda mrefu<br />

• Mwenye uwezo wa kupanga<br />

na kusimamia kazi yake<br />

• Mwenye ari ya kutafuta<br />

habari<br />

• Mwenye uwezo wa<br />

kushawishi na kutoa<br />

ushirikiano<br />

• Anaejiamini na kutenda<br />

Ijapokuwa watu wengi husema<br />

kwamba uwezo wa kijasiriamali ni<br />

kipaji cha kuzaliwa na huthubutu<br />

kufananisha na baadhi ya makabi<strong>la</strong><br />

yanayofanikiwa kibiashara kama<br />

vile, Wakikuyu-Kenya, Wahindi na<br />

Waarabu-Asia, Wachaga-Tanzania<br />

Bara na Wapemba-Zanzibar. Watu<br />

wengine husema Ujasiriamali<br />

unapatikana kwa kusomea, Je nani<br />

yuko sahihi kati ya wenye hoja mbili<br />

hizi?<br />

Utafi ti uliofanywa sehemu tofauti<br />

duniani haukubaliani na hoja ya<br />

kwanza pekee, kuwa mjasiriamali<br />

hamilikiwi na kundi fu<strong>la</strong>ni pekee<br />

Mjasiriamali anaweza kuekeza katika biashara yoyote ile bi<strong>la</strong> ya kujali kutokea kwa<br />

hasara, kinu cha kusagia nafaka ni moja ya biashara hizo.<br />

katika jamii bali mjasiriamali<br />

anaweza kutoka katika kabi<strong>la</strong><br />

na jamii yoyote duniani. Vile vile<br />

wata<strong>la</strong>mu wengi wanakubaliana<br />

kwamba Mjasiriamali akiwa na<br />

sifa zote mbili ndio muama<strong>la</strong> zaidi<br />

kuliko kuwa na kipaji cha kuzaliwa<br />

pekee.<br />

Ki<strong>la</strong> mtu anaweza kuwa mjasiriamali,<br />

cha muhimu ni kuamua, kujituma<br />

na kutenda. Baadhi ya wataa<strong>la</strong>mu<br />

wanasema hakuna mtu anaezaliwa<br />

mjasiriamali, bali watu wengi huiga<br />

au kujifunza ujasiriamali kutoka<br />

kwa waliowazunguka kama vile<br />

wazazi, walezi au kupitia mafunzo<br />

ya fani hiyo. Kwa mantiki hiyo,<br />

yeyote anaweza kuwa mjasiriamali<br />

na mwenye mafanikio makubwa ya<br />

kupigiwa mfano.<br />

USIMAMIZI NA UENDESHAJI WA<br />

BIASHARA ZA KILIMO<br />

Biashara za kilimo<br />

Zinajumuisha utaratibu mzima wa<br />

kupangilia matumizi ya pembejeo<br />

za kilimo ili kuweza kudhibiti na<br />

kutambua uhusiano baina ya<br />

13<br />

pembejeo zilizotumika na mazao<br />

yaliyopatikana katika kipindi<br />

cha uzalishaji. Utaratibu huu<br />

unahusiana na kuelewa uchumi<br />

wa kilimo na mbinu za ujasiriamali<br />

katika kumudu na kuendesha<br />

miradi midogo na mikubwa.<br />

Usimamizi na uendeshaji<br />

Ni utendaji wa kazi kwa kutumia<br />

mtu au kikundi cha watu pamoja<br />

na rasilimali nyingine kwa utaratibu<br />

maalum uliopangwa ili kuweza<br />

kufi kia malengo yaliyokusudiwa.<br />

Kazi za usimamizi na uendeshaji<br />

ni pamoja na kupanga, kuongoza,<br />

kuhamasisha, kuajiri, kudhibiti na<br />

kutathmini.<br />

Mambo muhimu ili msimamizi<br />

aweze kufanya kazi zake vizuri:<br />

• Awe mwenye kuielewa kazi<br />

yake vizuri<br />

• Atoe au kupata motisha<br />

• Afuate taratibu za sheria<br />

• Awe mwenye kufahamu<br />

mazingira ya kazi<br />

• Awe na uwezo wa kufanya


Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong> UJASIRIAMALI<br />

tathmini ya kazi<br />

Sifa za mjasiriamali katika<br />

kusimamia biashara:<br />

1. Kuweka malengo kwa<br />

usahihi na yawe mahsusi,<br />

yanayopimika, yanayofi kika,<br />

yanayofaa na yanayoweza<br />

kufuatiliwa.<br />

2. Kuwa na mfumo wa taarifa na<br />

kuweka kumbukumbu kama<br />

vile kudhibiti na kutathmini<br />

maendeleo, kufanya maamuzi<br />

na kupanga mipango ijayo,<br />

kuelewa mbinu mpya juu<br />

ya teknolojia, masoko na<br />

mazingira.<br />

3. Muda ni bidhaa muhimu kuliko<br />

bidhaa nyengine na kama<br />

muda hautunzwi hakutakua<br />

na maendeleo mazuri. Muda<br />

ni kigezo kikuu cha utendaji<br />

ukitunzwa huleta ufanisi.<br />

Kutunza muda ni kugawa muda<br />

huo kwa ajili ya kuweka malengo<br />

kwa umuhimu wake, kugundua<br />

na kuondosha vipoteza muda na<br />

kutumia maarifa ya uongozi ili<br />

kufi kia malengo kiufanisi zaidi.<br />

Mambo ya kuzingatia:<br />

• Hakuna namna ya kuweza<br />

kufi dia muda – Dakika<br />

moja iliyopotea haiwezi<br />

kurudi tena<br />

• Panga mambo yako kwa<br />

vipaumbele ili kuokoa<br />

muda<br />

• Hakuna muda mchache,<br />

kuona muda mchache ni<br />

dalili za uongozi mbaya<br />

• Ku<strong>la</strong><strong>la</strong> wakati wa usiku ni<br />

njia pekee ya kupumzika na<br />

sio kucheza gemu au kukaa<br />

maskani wakati wa mchana<br />

kama ndio njia muafaka ya<br />

kupumzika<br />

Mambo yafuatayo husababisha mtu<br />

kupoteza muda bi<strong>la</strong> kujijua au kwa<br />

kujua kwa maana ya kupumzika:<br />

• Kucheza gemu na kuandika<br />

ujumbe wa maandishi sana<br />

katika simu<br />

• Kupokea na kufurahia<br />

wageni wanaokuja bi<strong>la</strong><br />

miadi<br />

• Kutoweka malengo na<br />

vipaumbele vya kazi<br />

• Kucheza karata, draft na<br />

bao <strong>la</strong> kete wakati wa kazi<br />

• Dawati lililojaa karatasi bi<strong>la</strong><br />

mpango<br />

• Kutogawa kazi kikamilifu<br />

au kufanya kazi zinazoweza<br />

kufanywa na walio chini<br />

yako<br />

• Kufanya mambo mengi kwa<br />

wakati mmoja<br />

• Kushindwa kusema hapana<br />

au siwezi<br />

• Ukosefu wa nidhamu<br />

4. Motisha ni kitu chochote<br />

kinachohimiza juhudi katika<br />

kazi. Kwa kawaida binaadamu<br />

akipata motisha huongeza<br />

juhudi. Vifuatavyo ni vitu<br />

vitolewavyo ili kuongeza juhudi:<br />

• Motisha kwa wafanyakazi<br />

ni kama vile kumpandisha<br />

cheo, kupata bonasi<br />

yanapotokea mafanikio<br />

makubwa na ongezeko <strong>la</strong><br />

mshahara<br />

• Motisha kwa wateja ni<br />

kama vile kupunguza bei,<br />

usafi ri wa bure, nyongeza<br />

ya kitu juu ya bidhaa<br />

aliyonunua, huduma<br />

nzuri kwa mteja ukiwemo<br />

14<br />

ukarimu na uchangamfu.<br />

5. Mawasiliano kwa mjasiriamali<br />

ni njia pekee ya kupokea<br />

habari kwa haraka, husaidia<br />

wateja kuelewa huduma,<br />

biashara au bidhaa zitolewazo<br />

na kupokea maoni ya wateja.<br />

Usipoitangaza biashara yako na<br />

kutafuta taarifa itakua vigumu<br />

kuingia katika ulimwengu wa<br />

biashara, kama vile usemi<br />

maarufu usemavyo “BIASHARA<br />

ITANGAZWAYO NDIO ITOKAYO”<br />

Zipo njia tofauti za mawasiliano<br />

zinazotumiwa na wajasiriamali.<br />

Miongoni mwake ni :<br />

• Mawasiliano kwa<br />

maandishi kama vile<br />

mabango ya matangazo,<br />

barua, vipeperushi, ripoti,<br />

lebo za kwenye bidhaa<br />

humuwezesha mjasiriamali<br />

kuwasiliana na wateja<br />

wake au wadau wengine<br />

wa biashara.<br />

• Mawasiliano kwa njia ya<br />

maongezi kupitia mijada<strong>la</strong>,<br />

warsha, kongamano,<br />

semina na mikutano.<br />

Mjasiriamali anaweza<br />

kupata muda mzuri wa<br />

kuwasiliana na wateja kwa<br />

kushiriki kwenye mafunzo<br />

ya shamba darasa, sehemu<br />

za maonyesho ya bidhaa<br />

kama vile maonesho ya<br />

biashara na ya wakulima<br />

• Mawasiliano ya ishara kama<br />

vile ishara za uso, mikono,<br />

mabega na kichwa, njia<br />

hii hutumika kwa wateja<br />

au wadau wengine wa<br />

biashara mara nyingi njia<br />

hii hutoa ujumbe mzuri au<br />

mbaya. Hivyo mjasiriamali<br />

<strong>la</strong>zima awe makini na<br />

ishara atoazo mteja hata<br />

kama wateja wanawasiliana<br />

wao wenyewe wanapokuwa<br />

katika eneo <strong>la</strong> biashara.


RASILIMALI ZA MSITUNI Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />

UMUHIMU WA RASILIMALI ZA MSITUNI<br />

Na Nassor S. Mkarafuu<br />

Rasilimali za msituni zina uasili<br />

wa kibaiolojia zikijumuisha<br />

wanyama na mimea ya aina na<br />

rika tofauti yenye faida kwa maisha<br />

ya viumbe pamoja na huduma<br />

zinazopatikana msituni au ardhi<br />

inayotumika. Kuwepo kwa rasilimali<br />

hizi kunategemea uwepo wa msitu.<br />

Rasilimali za msituni zina faida<br />

nyingi kwa maisha ya viumbe<br />

wakiwemo binadamu, wanyama<br />

na wadudu. Miongoni mwa faida<br />

za moja kwa moja ni upatikanaji<br />

wa chaku<strong>la</strong>, miti ya mapambo,<br />

vichanganyisho vya manukato,<br />

mbegu pamoja na upatikanaji wa<br />

wanyama na mimea yenye kutoa<br />

tiba.<br />

Faida nyengine ni pamoja na<br />

uhifadhi wa vyanzo vya maji,<br />

kurekebisha hali ya hewa, ufyonzaji<br />

wa hewa mkaa, uhifadhi wa udongo<br />

na kuzuia mmong’onyoko, ambapo<br />

katika nchi nyingi za Afrika,<br />

rasilimali hizi zina umuhimu wa<br />

upatikanaji wa lishe kwa kaya.<br />

UTEGEMEZI WA JAMII KWA<br />

MAZAO YAPATIKANAYO MSITUNI<br />

Duniani kote jamii zinategemea<br />

rasilimali zinazopatikana msituni<br />

ikiwemo kujikimu kwa chaku<strong>la</strong>,<br />

malisho ya wanyama, madawa na<br />

zana za ujenzi. Matumizi mengine<br />

ni pamoja na kupatikana zana<br />

za ukulima, utengenezaji wa<br />

mapambo ya majumbani.<br />

Nchi nyingi za Afrika na Asia,<br />

jamii hutegemea rasilimali hizo<br />

kwa kuongeza kipato cha kaya,<br />

kupata uhakika wa chaku<strong>la</strong> na<br />

lishe, biashara na ajira kwa<br />

ujum<strong>la</strong>. Hata hivyo rasilimali hizo<br />

hazipewi umuhimu na wanasiasa<br />

na wapangaji wa mipango ya<br />

Maendeleo licha ya umuhimu wake,<br />

mara nyingi watu hutoa thamani<br />

ya msitu pale tu yanapopatikana<br />

mavuno yake, kuyatumia,<br />

kutengeneza bidhaa, kuziuza na<br />

kuchangia kuoengeza kipato kwa<br />

jamii za vijijini. Rasilimali hizi ni<br />

kiashirio kikubwa katika kupunguza<br />

Misitu huchangia katika upatikanaji wa rasilimali nyingi pamoja na umuhimu<br />

wake husaidia katika kuhifadhi mazingira na vyanzo vya maji.<br />

umasikini kwa jamii zinazotegemea<br />

msitu kwa kuongeza kipato, kupata<br />

uhakika wa chaku<strong>la</strong>.<br />

Uhakika wa Chaku<strong>la</strong> na Lishe<br />

Rasilimali za msituni zina mchango<br />

mkubwa katika kuchangia uhakika<br />

wa chaku<strong>la</strong> na lishe katika jamii<br />

kwa nyanja tofauti kama vile<br />

kupata chaku<strong>la</strong> kinachochangia<br />

kutoa vitamini, madini, uanga<br />

na protini muhimu. Jamii nyingi<br />

za vijjini zinatumia vyaku<strong>la</strong><br />

vinavyopatikana msituni kwa ku<strong>la</strong><br />

au kuuza kwa lengo <strong>la</strong> kupata pesa<br />

za kununulia chaku<strong>la</strong> hasa wakati<br />

wa uhaba wa mavuno ya mazao<br />

mashambani. Miongoni mwa<br />

mazao yanayopatikana msituni<br />

ni pamoja na matunda, mboga<br />

mboga, wanyama pori na asali.<br />

Matunda<br />

Mabungo, Zambarau, Fuu, Ukwaju,<br />

Ubuyu, Mapera, Pilipilidoria, Maviru,<br />

Kunazi na Chongoma. Aidha, katika<br />

baadhi ya nchi za Afrika mazao<br />

kama edible nuts zinatumika kwa<br />

chaku<strong>la</strong>, mafuta ya ku<strong>la</strong>, viungo,<br />

achari na vinywaji.<br />

Mbogamboga<br />

15<br />

Miongoni mwa mboga<br />

zinazopatikana ni kikwayakwaya,<br />

pwipwi, mchicha mwiba, mchunga,<br />

mronge, mchambale, mboga ya<br />

pwani na mnavu. Aina hizi za mboga<br />

za asili zinatoa madini mengi zaidi<br />

kuliko aina ya mboga zisizokuwa za<br />

asili. Inasemekana mboga za asili<br />

zina madini ya chokaa (calcium)<br />

1.5 – 3.2 zaidi ya mboga mboga za<br />

jamii ya kabeji ambazo ndizo zenye<br />

madini ya chokaa (calcium) nyingi<br />

kwa mboga zisizokuwa za asili.<br />

Wanyama pori<br />

Wanyama pori ni miongoni mwa<br />

chaku<strong>la</strong> muhimu katika kuongeza<br />

uhakika wa chaku<strong>la</strong> na lishe<br />

wakijumuisha wanyama, ndege<br />

na mayai yao pamoja na samaki.<br />

Nyama itokanayo na wanyama<br />

hawa ni chanzo cha protini na<br />

madini mengine kama chuma,<br />

vitamin A na B. Wanyama wadogo<br />

(paa) na ndege (kanga) ni maarufu<br />

katika kuongeza chaku<strong>la</strong> na lishe<br />

ya jamii.<br />

Asali<br />

Ni miongoni mwa chaku<strong>la</strong> maarufu<br />

hapa nchini. Kawaida asali iliyo<br />

nyingi hutengenezwa na nyuki<br />

na hupatikana msituni baada ya


Toleo <strong>la</strong> Saba<br />

Ju<strong>la</strong>i - <strong>Septemba</strong>, <strong>2011</strong><br />

kuvunwa ambayo hutumika katika<br />

jamii kwa ku<strong>la</strong>, dawa na biashara.<br />

miongoni na Faida nyengine,<br />

masega ya nyuki hutumika katika<br />

kutengeneza mshumaa na maji<br />

maji yaitwayo royal jelly.<br />

Matumizi ya asali yanatofautiana<br />

kutoka sehemu moja hadi nyengine<br />

kutokana na upatikanaji na hali<br />

ya soko. Wananchi wa vijijini mara<br />

nyingi hutumia asali kama dawa ya<br />

kutibu maradhi mbali mbali pamoja<br />

na kuuza kwa kujiongezea kipato.<br />

Hapa Zanzibar lita moja inauzwa<br />

kwa wastani wa shilingi 12, 000.<br />

Hii inamaanisha kwamba asali<br />

ni moja kati ya rasilimali yenye<br />

umuhimu katika afya na kuongeza<br />

kipato katika jamii.<br />

Dawa za asili<br />

Dawa za asili ni mazao muhimu<br />

yanayopatikana kutoka msituni<br />

ambapo nchi zote za Afrika<br />

zinatumika. Zaidi ya watu bilioni<br />

3.5 wanaoishi pembezoni mwa<br />

misitu duniani wanatumia dawa<br />

za asili na inakisiwa aina 35,000<br />

zinatumika ambapo katika nchi<br />

za Afrika zaidi ya asilimia 80 ya<br />

watu wanatumia dawa za asili kwa<br />

matibabu ya maradhi na maumivu<br />

mbali mbali. Shirika <strong>la</strong> Afya Duniani<br />

(WHO) limekisia kwamba zaidi ya<br />

asilimia 80 ya watu katika nchi<br />

zinazoendelea wanategemea dawa<br />

za asili kwa matibabu ya msingi na<br />

zinapatikana kwa urahisi na jamii<br />

inazifahamu.<br />

Miongoni mwa miti ya dawa<br />

maarufu zinazotumika hapa nchini<br />

ni pamoja na Mchofu, Mvuje,<br />

Mtarawanda, Kivumbasi, Mwavikali<br />

na Mpande ambazo zinatumika<br />

kwa kutibu maradhi mbali mbali<br />

kwa binadamu yakiwemo maradhi<br />

ya tumbo, kichwa, ngiri pamoja<br />

Kima punju ni miongoni mwa rasilimali ya msituni ambayo ni kivutio kikuu cha<br />

Msitu wa Hifadhi wa Jozani kwa watalii wa ndani na wa nje ya nchi.<br />

na maradhi ya matumbo ya<br />

kinamama.<br />

Miti ya mapambo<br />

Miti hii inatumika maalumu kwa<br />

ajili ya mapambo katika maeneo<br />

inayoishi jamii na kupendezesha<br />

hali ya mandhari. Jamii nyingi<br />

zinatumia miti hii katika nyumba<br />

zao au katika sehemu ambazo watu<br />

hupenda kupumzika na kwenye<br />

mahoteli za kitalii. Miongoni mwa<br />

miti maarufu inayotumika kwa<br />

mapambo inayopatikana msituni<br />

ni pamoja na Mgwede, Mkonge,<br />

Mkuyu na Mnunu ambayo pamoja<br />

na kutumika kwa mapambo pia<br />

hutumika kwa kutoa kivuli.<br />

Uhifadhi wa vyanzo vya maji<br />

Maji ni rasilimali za misitu<br />

zinazosaidia uzalishaji wa bidhaa<br />

mbali mbali na kuongeza pato <strong>la</strong><br />

taifa na yanasaidia kwa afya ya<br />

binaadamu. Maji ya mito, maziwa,<br />

mvua na sehemu za unyevu ni<br />

vyanzo muhimu vya uzalishaji wa<br />

mazao. Misitu inasaidia kuhifadhi<br />

kina cha maji, kupatika kwa<br />

uhakika na kupunguza chumvi<br />

katika maji. Aidha, miti inatoa nafasi<br />

ya makaazi ya samaki. Majani<br />

na magogo yalioza yanaongeza<br />

virutubisho kwa viumbe waishio<br />

majini.<br />

Rasilimali zinazopatikana msituni<br />

ni muhimu na zinahitaji kuwekewa<br />

mkakati maalum wa kuziendeleza<br />

na kuzitunza kwa vile zinachangia<br />

kustawisha uchumi wa nchi kwa<br />

kuongeza pato <strong>la</strong> taifa na usitawi<br />

wa maisha ya mwanadamu pamoja<br />

na viumbe vyengine. Aidha, taasisi<br />

zinazohusika ni vyema kufanya<br />

utafi ti na kuweza kuzitangaza<br />

rasilimali hizi na kuzianisha kwa<br />

jamii na matumizi yake.<br />

GAZETI HILI HUTOLEWA KILA BAADA YA MIEZI MITATU NA<br />

WIZARA YA KILIMO NA MALIASILI - ZANZIBAR<br />

P. O. Box 159 Zanzibar, Simu: +255 24 2230986, Fax: +255 24 2234650<br />

Barua pepe: kilimo@zanlink.com, Tovuti: www.kilimoznz.or.tz

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!